Kim Kardashian.
New York, MarekaniBAADA ya kujifungua mtoto wa kiume juzi (Jumamosi), mashabiki wa mwanamitindo na mtangazaji maarufu wa Kipindi cha Keeping Up With The Kardashian, Kim Kardashian wameibuka katika mitandao ya kijamii na kumtaka Kim kumuita mtoto huyo jina la Easton West.
Kim Kardashian akiwa na mumewe Kanye West.“Najua ataitwa tu Easton West.”
“Natamani kweli aitwe Easton West.”
Zilisomeka baadhi ya meseji hizo kwenye ukurasa wa Twitter.
TAngu Kim ana ujauzito wa mtoto huyu aliyejifungua jana, hakuwahi kuweka wazi jina la mtoto hali inayoendelea kuzua sintofahamu kwa mashabiki wake baada ya mtoto wake wa kike wa kwanza kumuita North West.

Post a Comment