MSANII wa filamu Bongo, Alice Bagenzi ‘Rayuu’ amefungukia ishu ya mastaa
wengi kupenda kwenda kujiuza nchi za nje ikiwemo Sauzi akisema kuwa,
wanaofanya hivyo hawajitambui na kinachowasumbua ni tamaa ya pesa.
Akipiga
stori na paparazi wetu hivi karibuni, Rayuu alisema alishasumbuliwa na
wadada wengi wakimpa madili ya kwenda kujiuza China, Sauzi na kwingineko
lakini akawatolea nje kutokana na msimamo alionao
“Unajua hakuna
kinachowapeleka huko zaidi ya tamaa kwa kuwa kule wanalipwa kwa dola
wakirudi huku wakizibadilisha wanapata pesa nyingi, halafu huku unakuta
mtu ameshatembea na wanaume wengi ndiyo maana anakimbilia nje,” alisema
Rayuu
Post a Comment