DAR ES SALAAM: Baada ya hivi karibuni Video Queen Asha Salum ‘Kidoa’
kuibuka na kueleza kuwa, yuko tayari kufanya lolote ili awe na
mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond’ kimapenzi, mdada huyo amenaswa tena
juzikati akiwa na mwanasoka Mbwana Samatta hotelini.
Mishale ya saa 5.30 usiku, chanzo chetu kilichokuwa maeneo ya Hoteli ya
Girrafe iliyopo Mbezi jijini Dar Jumapili iliyopita, kilitutonya kuwa
kilikuwa kikiwaona wawili hao wakizama hotelini hapo bila kujulikana
kilichowapeleka.
“Ee
bwana nipo hapa Girrafe Hoteli, ila naomba nisijulikane kama nimewapa
taarifa, ni hivi muda mrefu nimemuona Mbwana Samatta na yule mrembo
mwenye makalio makubwa sijui anaitwa Kidoo….
Ijumaa: Siyo Kidoo, anaitwa Kidoa.
Chanzo: Ndiyo, huyo huyo.
Ndiyo nawaona wako katika eneo la restaurant (hotelini), kama ni habari kwenu njooni mtawakuta.
Ijumaa: Wako katika mazingira gani?
Chanzo: Naomba kama mnahitaji habari mje tu usiniulize maswali mengi maana nitashitukiwa, wahini kabla hawajaondoka.
Ijumaa: Oke, poa tunakuja
Baada ya kupata taarifa hiyo, waandishi wetu walichukua usafiri wao wa
pikipiki ziendazo kasi na kuanza safari ya kuelekea Mbezi.
Wakati paparazi wetu wakielekea eneo la tukio, simu ya mmoja wao ikaita, alikuwa yule sosi wa habari hiyo.
Kidoa na Samata wakiondoka hotelini.
Chanzo:
Mbona mnachelewa? Naona wanainuka kama wanataka kuondoka hivi.
Wanaonekana kuwa wenye furaha sana. Naona wanapiga picha, Kidoa
anamsogelea. Kwa kifupi wanafanya yao.
Ijumaa: Hebu wafotoe picha hata kwa kamera ya simu yako.
Chanzo: Sawa, ngoja nijaribu kufanya hivyo.
Saa 6 usiku
Mishale ya saa sita usiku, paparazi wetu wakawa wamefika hotelini hapo
na kukuta wawili hao wakiingia kwenye gari aina ya Toyota Mark X nyeusi
kisha kuondoka zao kuelekea kusikojulikana.
Wenyewe wanasemaje?
Jitihada za kuwasaka mastaa hao zilifanyika ambapo Samatta hakuweza
kupatikana kupitia simu yake ya mkononi lakini Kidoa alipopatikana
alikiri kufika hotelini hapo kwa mazungumzo ya kawaida na mwanasoka huyo
aliyejipatia umaarufu mkubwa.
“Ni
kweli tulienda pale, hakukuwa na chochote zaidi ya mazungumzo ya
kawaida tu na tuliishia restaurant tu, hakuna lolote. Yule najuana naye
muda mrefu mbona, msidhani nampapatikia kwa sababu ya tuzo aliyopata,”
alisema Kidoa.
Hivi
karibuni, Samatta aliitoa kimasomaso Tanzania baada ya kushinda tuzo ya
Mwanasoka Bora wa Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani,
iliyofanyika nchini Nigeria na kuweka historia ya kuwa Mbongo wa kwanza
kupata heshima.
Post a Comment