Mtanzania anayekipigia klabu ya Genk ya nchini Ubelgiji ameendelea kuwika baada ya usiku wa leo kuweza kuifungia moja ya mabao klabu yake hiyo ambayo iliibuka na ushindi wa bao 4-1 dhidi ya wapinzani wao Oostende.
Ushindi huo wa leo Machi 13.2016, Kwa Mtanzania Mbwana Samatta anakuwa anafikisha magoli mawili (2) tokea alipojiunga na timu hiyo. Ushindi huo unakuwa wa pili dhidi ya Mbwana Samatta tokea kujiunga na klabu hiyo.
Imeandaliwa  na Andrew Chale, Modewjiblog, Kwa msaada wa mashirika ya Habari.
Kuona video hiyo bonyeza hapa:


samatta-genkMtanzania Mbwana Samatta akishuhudia mpira alioudumbukiza golini wakati wa  bao lake hilo kayika mchezo uliochezwa leo usiku huu.