Imebainika
kuwa Tanzania inakabiliwa na changamoto ya kuwaajiri mahotelia wasio
kuwa na ujuzi wa kutosha katika sekta ya utalii haswa kwenye hoteli
hali ambayo inarudisha nyuma uchumi wa nchi tofauti na nchi
nyinginezo za nje ya nchi.
Hayo
yalisemwa na Meneja mkazi wa kampuni ya Jovago Tanzania, Andrea Guzzoni
alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari katika uzinduzi wa ripoti
ya mwisho yenye utafiti inayohusiana na sekta ya utalii ili kuweka wazi
hali inayoikabili sekta hiyo.
Alisema
kuwa sekta ya utalii kwa hapa Tanzania imekuwa ikipanda na kushuka
mwaka hadi mwaka lakini bado ina changamoto ya kuwaajiri wafanyakazi
kwa mazoea badala ya kuwaajiri wenye ujuzi wa kutosha hali ambayo
amesema kuwa inapaswa kuangaliwa kwa upya ili kuiwezesha sekta hiyo
kupanda kiuchumi.
Aliongeza
kuwa ili Tanzania iweze kufikia watalii milioni mbili miaka ijayo
serikali inapaswa kuangalia utaratibu wa kuwachukua mahotelia na
kuwapeleka nje ya nchi ili waweze kujifunza jinsi ya kuhudumia wageni
kwani wapo wengine ambao hawajui lugha na hata jinsi ya kuhudumia wageni
wanaongia nchini hali inayowafanya watalii kukosa huduma nzuri.
Aidha
Guzzoni aliwataka wadau wote ndani ya sekta ya utalii kuhakikisha
wananchangamkia fursa ya kujitangaza na kuonyesha utofauti wao kwa
umahiri ili kusaidia watanzania wenye nia na maendeleo na utalii wa
ndani.
Kwa
upande wake Afisa Habari na Uhusiano wa kampuni hiyo, Lilian Kisasa
akizungumza katika uzinduzi huo alisema kuwa kwa hapa Tanzania sekta ya
utalii imeweza kuajiri watu zaidi ya laki sita na endapo huduma nzuri
zitaboreshwa katika sekta hiyo upo uwezekano wa kuajiri watu zaidi ya
hapo jambo ambayo itapunguza hata tatizo la ajira hapa nchini.
Afisa habari na uhusiano wa kampuni Jovago Tanzania Lilian Kisasa na Meneja mkazi wa kampuni ya Jovago Tanzania Andrea Guzzoni katika uzinduzi huo.
Meneja mkazi wa kampuni ya Jovago Tanzania, Andrea Guzzoni alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari katika uzinduzi wa ripoti ya mwisho yenye utafiti inayohusiana na sekta ya utalii ili kuweka wazi hali inayoikabili sekta hiyo.
Afisa habari na uhusiano wa kampuni Jovago Tanzania, Lilian Kisasa akizungumza katika uzinduzi huo ambapo alisema hapa Tanzania sekta ya utalii imeweza kuajiri watu zaidi ya laki sita na endapo
huduma nzuri zitaboreshwa katika sekta hiyo upo uwezekano wa kuajiri watu zaidi ya hapo jambo ambalo litapunguza hata tatizo la ajira hapa nchini.(Pamela Mollel jamiiblog)
huduma nzuri zitaboreshwa katika sekta hiyo upo uwezekano wa kuajiri watu zaidi ya hapo jambo ambalo litapunguza hata tatizo la ajira hapa nchini.(Pamela Mollel jamiiblog)
Wanahabari wakiwa katika uzinduzi wa ripoti.
Post a Comment