Juma Nature asema haya kuhusu wasanii wanaotumia unga

13388569_1132649460091171_1422662606_n
Alikiri kuyatumia kwa mwaka na nusu na kwamba ameacha huku akiahidi maisha mapya na kupendeza zaidi akiwa tena chini ya uongozi wa label ya MDB.
Rapper Juma Nature ametoa maoni yake pia kuhusiana na matumizi ya madawa hayo.
“Kuna mambo ambayo nikijiuliza jibu sipati hivi ni kweli kuna wasanii wanakula mambo hivi, mbona sisi uhuni tumepitia lakini lakaya hii nimpya,” aliandika kwenye Instagram.
“Punguzeni kuiga wadogo zng jamii inawategemea…maana hatatukisema tuwaombeee kazi bure mtarudia tu! Kwani huyo anayewauzia anawashikia bastora ndg zng? Misijapendezwa namichongo famfa kujiendekeza banaaaaa,” aliongeza.
Matumizi ya madawa ya kulevya kwa wasanii yamekuwa hadithi isiyoisha huku Chidi Benz na Ray C wakiwa wahanga waliotawala zaidi headlines kwa sasa.

Post a Comment

Previous Post Next Post