Wizara ya Mifugo yapanga kukifufua kituo cha upandishiaji wa ngombe Zanzibar


Wizara ya Mifugo na Uvuvi Zanzibar iko katika harakati za kukifufua upya Kituo cha kupandishia Ngombe kilichopo katika eneo la Maruhubi nje kidogo ya Mji wa Zanzibar ili kirejee katika utaratibu wake wa kutoa huduma bora kwa wafugaji wa Ngo’mbe wa kisasa hapa Nchini.

Kituo hichoanzishwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar mwanzoni mwa miaka ya 70 na kusitisha huduma zake kutokana na mabadiliko ya sera ya ufugaji kwa kuachiliwa suala hilo kuendeshwa na wananchi moja kwa moja.

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Zanzibar Dr. Kassim Gharib alieleza hayo wakati wa ziara fupi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi aliyefika katika eneo hilo kukagua juhudi zinazochukuliwa na Wizara hiyo katika kukifufua tena kituo hicho.

Dr. Kassim alimueleza Balozi Seif kwamba Wizara hiyo imeanza na hatua ya kuzunguusha ukuta eneo hilo ili kuzuia uvamizi wa ujenzi holela wa nyumba pamoja na uchimbwaji ovyo wa mchanga uliokuwa ukitishia uchafuzi wa mazingira.

Alisema hatua hiyo itakapokamilika itatoa fursa kwa wafanyakazi wa Mifugo kuendelea na hatua ya pili ya upandaji majani kwa ajili ya malisho ya madume ya ng’ombe watakaotumiwa kutoa mbegu na kuendelea kusambazwa kwa wafugaji kwenye maeneo mbali mbali nchini.

Dr. Kassim alifahamisha kwamba licha ya matatizo na changamoto mbali mbali zilizokuwa zikikikabili kituo hicho lakini bado kinaendelea kutoa huduma za upandishiaji ng’ombe kikiwa na Madume Sita bora ya kisasa hivi sasa.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif pia alipata fursa ya kukagua kara kana inayohudumia matengenezo ya dharura ya vyombo vya moto vya Wizara hiyo ya Mifugo na Uvuvi iliyopo jirani na kituo hicho.

Othman Khamis Ame 
 Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar 

Post a Comment

أحدث أقدم