Mwimbaji wa muziki wa dansi kutoka Congo, Christian Bella
amepanga kuachia wimbo wa mahadhi ya R&B hivi karibuni ambao ameuita
‘Utamtaka’.
“Kuna R&B moja sasa natoa ya kwangu, naimba sasa R&B na
nimeiandika mimi…utaisikia hiyo mwanangu.” Christian Bella ameiambia
tovuti ya Times Fm.
“Nimeshatengeneza beat nadhani mpaka next week naiimba, ntaiweka
kwenye albam yangu ntakuwa na mastyle tofauti tofauti naenda kuingiza
sauti next week. Nimefanya kwa C9. Ukiwa msanii lazima uonje
style tofauti tofauti, lazima uoneshe ubunifu kwamba unaweza kufanya
style zote.
“Ukisikiliza albam yangu ya Don’t Panic nilijaribu kufanya RnB
fulani niliimba Africa. Ilikuwa kama RnB lakini, niliimba Africa Stand
up na nilirap pia ndani. Mimi kila siku najaribu kufanya kitu ambacho
sio utaarabu wangu ambao naimba. Naangalia pia beat nyingine pia nafanya
nikiwa na albam watu wanasikiliza rhumba, mtu akisikiliza RnB mtu
anaependa RnB anajikuta. Napiga ngoma msanii wa hip hop, unashirikisha
msanii wa bongo flava”.
Christian Bella hivi ambaye alikuwa anafanya kazi na bendi ya Akudo Impact, hivi sasa anafanya kazi na bendi ya Malaika.
Msikilize hapa akieleza na kutoa kionjo cha wimbo huo.
إرسال تعليق