Ujumbe toka Afrika, Mashariki ya Kati na Ghuba ya Uajemi wawasili Marekani

Ujumbe toka Afrika, Mashariki ya Kati na Ghuba ya Uajemi wawasili Marekani

Ujumbe toka Afrika, Mashariki ya Kati na Ghuba ya Uajemi ukiongozwa na Rais wa IBF-Africa Mtanzania Onesmo Ngowi umewasili katika uwanja wa ndege wa Oahu, jiji la Honolulu, Hawaii na kulakiwa na Mstahiki Meya wa jiji la Hawaii Peter Carlisle. 

Ujumbe huo unajumuisha wawakilishi toka Afrika ya Kusini, Botswana, Uganda, Ghana, Nigeria, Oman, UAE (Dubai), Jordan, Gabon, Morocco, Ivory Coast na Tanzania.

Jana, ujumbe huo ulifanya mazungumzo na Mstahiki Meya wa jiji la Los Angelos, Antonio Villaraigosa katika chumba cha watu mashuguri (VIP) kwenye uwanja wa ndege wa Los Angelos na kuzungumzia masuala ya Utalii katika Afrika, Mashariki ya Kati na Ghuba ya Uajemi.

Meya Villaraigosa aliahidi kuwahamasisha watu wa Los Angelos kutembelea  na kuwekeza katika ukanda huu na kuukaribisha ujumbe huo kulitembelea jiji la Los Agelos mwezi wa tida kwaka huu.

Wajumbe toka Botswana, Afrika ya Kusini, Oman,  Jordan na UAE (Dubai) wamefuatana na wafanyabishara wa Utalii (Tour Operators).

Mkutano mkuu wa IBF/USBA utafanyika katika hotel ya Hawaii Hilton Village katika mji mdogo wa Waikiki, jiji la Honolulu, Hawaii, Marekani. Huu ni mkutano unaohudhuriwa na wajumbe zaidi ya 6000 toka nchi 204 duniani.

Hawii Hilton Village ipo kwenye eneo la hekari 28 ambapo kuna majengo na maduka makubwa ya bidhaa mbalimbali. Hapa ndipo IBF itafanya mkutano wake wa mwaka wa 29. Hapa ndipo ujumbe toka Afrika, Mashariki ya Kati na Ghuba ya Uajemi utatoa mpango wake wa Utalii wa Michezo (Sporst Tourism).

Ujumbe wa bara la Afrika, Mashariki ya Kati na Ghuba ya Uajemi uko hapa kutangaza biashara ya utalii ili kuweza kuwanasa watalii wengi wanaotoka sehemu mbalimkbali duniani na wanaohudhuria kwenye mkutano huu. Mkutano huu utaanza rasmi tarehe 29 Juni, 2012.

Jimbo la Hawaii linajulikana kwa wengi kutokana na umaarufu wake katika vita vya pili vya dunia wakati Wajapani na Manazi waliposhambulia Pearl Habor mwaka 1941 ambapo iliilazimu Amerika ambayo kwa wakati huo ilikuwa haina upande (Neutral) kujiunga na vita ya pili ya dunia ambapo baadaye ilimalizika!

Post a Comment

أحدث أقدم