WAZAZI NCHINI KENYA HATARINI KUFUNGWA JELA IWAPO WATASHINDWA KULIPA ADA ZA SHULE.

Wazazi watakaoshindwa kuwapeleka shule watoto wao nchini Kenya watakuwa katika hatari ya kuhukumiwa kifungo cha jela iwapo mswada mpya uliowasilishwa utapitishwa kuwa sheria.
Mswada huo unapendekeza mzazi kupigwa faini ya shilingi 5,000 ya Kenya au kufungwa jela kwa muda wa mwaka mmoja.
Katika hatua nyingine mitihani ya majaribio itazuiliwa na hakuna mwanafunzi atakayenyimwa kuingia katika shule yeyote ya msingi ya serikali.
Hata hivyo mwanafunzi yeyote atayeshindwa kuendana na utaratibu wa shule kutokana na sababu za kiakili, kimaumbile au kisaikolojia anaweza kuondolewa kwa kibali cha Waziri wa Elimu.
Mswada huo uliochapishwa na Waziri wa Elimu Mutula Kilonzo umeandaliwa baada ya kufanyika kwa mfululizo wa mashauriano.
Kwanza wizara ya elimu iliunda kikosi kazi chini ya Makamu wa Rais wa Chuo Kikuu cha Moi Profesa Douglas Odhiambo, ambacho kiliandaa ripoti ambayo ilipitiwa katika mkutano wa kitaifa wa wadau wa elimu uliofanyika mwezi Machi jijini Nairobi.

Post a Comment

أحدث أقدم