WAZIRI WA HABARI AZINDUA MUONGOZO NA KANUNI KWA WAMILIKI NA MAMENEJA WA VYOMBO VYA HABARI

Meneja Mkuu wa Kampuni ya Global Publishers, Abdalah Mrisho (wa pili kushoto) akiwa na wajumbe wenzake wa  Kamati ya Maandalizi ya mkutano huo, wakiandaa mazingira kabla ya mkutano huo kuanza. Wa kwanza kulia ni Bi. Joyce Mhavile wa ITV/Radio One, anayemfuatia ni Masoud Sanani wa Business Times na wa kwanza kushoto ni Hamza Kasongo wa Channel Ten.
Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP na Mwenyekiti wa Chama Cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari nchini (Moat), Reginald Mengi, akifungua mkutano huo.
Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Dk. Emmanuel Nchimbi, akitoa hotuba na kuwasifu wamiliki wa vyombo vya habari nchini kwa kuamua kwa hiyari yao kuanzisha muungozo huo.
Waziri Nchimbi akiweka saini makubaliano hayo na Mwenyekiti wa Moat, Reginald Mengi (kulia) na Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya kuendeleza Vyombo vya Habari Afrika (AMI), Amadou Mahtar Ba.
Wakijadiliana jambo baada ya kutiliana saini makubaliano hayo.
Waziri Nchimbi na Mengi wakiwa na nyuso za furaha wakati wakiteta jambo.
Mwenyeki wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, akichangia mada wakati wa mjadala wa kuboresha taaluma ya habari.
Mwanasiasa  maarufu nchini, Prince Bagenda naye akichangia hoja.
Wajumbe wa Kamati ya Maandalizi ya uzinduzi wakiwa katika picha ya pamoja. Kutoka kulia, Henry Muhanika (Katibu), Masoud Sanani (Mjumbe), Abdallah Mrisho (Mjumbe), Theophil Makunga (Mwenyekiti) na Hamza kasongo (mjumbe).Mwenyekiti wa Moat, Reginald Mengi, akiongea na wanahabari baada ya kutiliana saini makubaliano hayo.
Ulipowadia wakati wa maakuli.
Wamiliki na mameneja wa vyombo vya habari nchini leo wametiliana saini mbele ya  Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo, Dkt. Emmanuel Nchimbi, makubaliano ya hiyari ya kuanzisha na kulinda Muungozo na kanuni za kuendesha vyombo vya habari nchini na nchi zingine barani Afrika. Makubaliano hayo yalisainiwa kwenye mkutano wa uzinduzi uliofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam. Katika mkutano huyo mijadala mbalimbali ya kuboresha taaluma ya habari ilijadiliwa.
Chanzo:-  globalpublishers

Post a Comment

أحدث أقدم