Mafisango kuenziwa Julai 8

MECHI ya hisani kati ya Simba na APR ya Rwanda ya kuichangia familia ya aliyekuwa kiungo wa kimataifa wa Rwanda, Patrick Mutesa Mafisango aliyefariki Aprili 17, itachezwa Julai 8, kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga, uhakika wa mechi hiyo umetokana na kufahamika kwa tarehe ya kuanza michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (Cecafa).
“Mechi ya hisani itachezwa Julai 8 kwenye Uwanja wa Taifa kwani tayari tumeshajua tarehe ya kuanza kwa michuano ya Kombe la Kagame,” alisema Kamwaga na kutoa wito kwa wapenzi wa soka kumuenzi nyota huyo kwa kufika uwanjani siku hiyo.
Aidha, klabu ya Simba imeweka kibao cheusi kwenye mti uliopo eneo la ajali iliyogharimu uhai wa nyota huyo, kikiwa na maneno yasemayo ‘Burian Mafisango’ na tarehe ambayo ajali hiyo ilitokea.
Kamwaga alisema kwa sasa wanafuaatilia kibali Manispaa ya Temeke wakitaka kuweka alama mahali hapo na kusema, kibao hicho kimewekwa na marafiki zake wa mtaani kwake, Chang’ombe

Post a Comment

أحدث أقدم