MAJERUHI WAONGEZEKA STARS, KIM POULSEN AELEZA MIKAKATI YA KUUA MAMBA

MAJERUHI WAONGEZEKA STARS, KIM POULSEN AELEZA MIKAKATI YA KUUA MAMBA


Kim Poulsen

KOCHA Mkuu wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Mdenmark Kim Poulsen amesema kwamba kipa Mwadini Ally na beki Waziri Salum wameingia kwenye orodha ya wachezaji majeruhi katika kikosi chake, wakati akijiandaa na mechi dhidi ya Msumbiji, ‘Mambas’ kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika mwakani Afrika Kusini.
Stars ambayo itacheza na Mambas Juni 17, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Zampeto nje kidogo ya Jiji la Maputo kuanzia saa 9 mchana kwa saa za huko, mechi ya kwanza ilitoka sare ya 1-1 na Msumbiji, Dar es Salaam na katika mchezo huo inatakiwa lazima ishinde au itoke sare ya zaidi 2-2 ifuzu kwa faida ya bao la ugenini.
Akizungumza na Waandishi wa Habari mchana wa leo leo, ofisi za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Poulsen amesema maandalizi ya kikosi chake yanakwenda vizuri ingawa Mwadini Ali na Waziri Salum wameungana na Naasor Masoud ‘Chollo’ katika ‘meza ya majeruhi’ na hawatakuwemo kwenye msafara wa timu hiyo utakaoondoka Juni 15 mwaka huu saa 11 alfajiri kwa ndege ya Kenya Airways kupitia Nairobi.
Kocha huyo amesema baada ya mechi tatu maendeleo kiuchezaji kwa timu yake inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ni mazuri ingawa bado anafanyia kazi kwa nguvu safu ya ushambuliaji. Mechi iliyopita Taifa Stars iliifunga Gambia 2-1 huku mabao yote yakifungwa na mabeki.
Iwapo Taifa Stars itaitoa Msumbiji katika raundi ya mwisho itapangiwa moja kati ya timu 16 zilizocheza Fainali za AFCON zilizofanyika Januari mwaka huu katika nchi za Gabon na Equatorial Guinea. Katika mechi ya kwanza dhidi ya Msumbiji iliyochezwa Dar es Salaam, Februari 29 mwaka huu timu hizo zilitoka sare ya bao 1-1.
Taifa Stars ambayo msafara wake utakuwa na wachezaji 20 itaagwa kesho (Juni 14 mwaka huu) saa 6 mchana kambini kwao- hoteli ya Accommondia (Tansoma) jijini Dar es Salaam.  Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) kwa ajili ya kujenga afya kupitia mpira wa miguu.

Post a Comment

Previous Post Next Post