Mbowe amkamia Membe Bungeni

KIONGOZI wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, ameahidi kuwakaba koo mawaziri wawili wa serikali ya Jakaya Kikwete katika Bunge la bajeti linalotarajiwa kuanza Juni 12 mwaka huu kwa kushindwa kutatua kero zinazowakabili Watanzania wakati uwezo huo wanao.
Mawaziri watakaokumbana na kibano cha Mbowe ni Bernad Membe, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Hawa Ghasia, Waziri Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).
Mbowe aliahidi kuwabana mawaziri hao juzi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Makanga wilayani Nanyumbu na kuhudhuriwa na maelfu ya wakazi wa wilaya hiyo ambao walitoa kero mbalimbali zinazowakabili.
Miongoni mwa kero hizo ni pamoja na kunyanyaswa pindi wanapotumia daraja la umoja kati ya Tanzania na Msumbiji kwa ajili ya kwenda nchi jirani ya Msumbiji hata kama wana vibali vya kuingia nchini humo.
Akielezea namna daraja hilo lisivyowanufaisha Watanzania na badala yake kuishia kunyanyaswa, Mkazi wa Makanga, Mkapura Omar, alisema tatizo hilo lilishamkuta yeye pamoja na Watanzania wengine ambao mpaka leo wako nchini Msumbiji kwa kushindwa kurudi baada ya kunyang’anywa kila kitu walichokuwa nacho ikiwamo vibali vya kuwaruhusu kuingia nchini humo.
Tunaomba mtusaidie; tunaonewa sana tunapotumia daraja la Umoja kwenda Msumbiji, mimi nilikwenda kuwasalimia ndugu zangu; nikafuata taratibu zote lakini nilipofika nikanyang’anywa kila kitu na askari wa Msumbiji licha ya kuwa na vibali halali vya kuingia katika nchi hiyo,” alisema Omary.
Akielezea hali hiyo Mbowe alisema hayo ni matokeo ya sera mbovu ya mahusiano ya kimataifa zinazowafanya Watanzania kunyanyaswa wanapokuwa mipakani.
Kuhusu viongozi wa serikali za mitaa wakiwamo madiwani na wenyeviti wa vijiji kutofanya mikutano na kuwasomea wananchi kile walichokitekeleza, Mbowe alisema kisheria wanawajibika kufanya hivyo kila baada ya miezi mitatu na atamhoji waziri Ghasia ili kujua hatua alizokwishachukua

Post a Comment

أحدث أقدم