MREMBO LISA JENSEN ANYAKUA TAJI LA REDDS MISS WORLD TANZANIA USIKU HUU, KUWAKILISHA TANZANIA MISS WORLD

MREMBO LISA JENSEN ANYAKUA TAJI LA REDDS MISS WORLD TANZANIA USIKU HUU, KUWAKILISHA TANZANIA MISS WORLD

Mrembo Lisa Jensen akipunga mkono kwa wapenzi wa masuala ya urembo waliohudhuria katika shindano dogo  la Redds Miss World Tanzania lililofanyika usiku wa kuamkia leo kwenye jiji la Dar es salaam na kushirikisha warembo 10 waliowahi kushiriki mashindano hayo  miaka mbalimbali iliyopita, Lisa Jensen atawakilisha Tanzania katika shindano la Miss World  litakalofanyika nchini Mongolia mwishoni mwa mwaka huu
Miss Tanzania Salha Israel akimvisha taji mrembo Lisa Jensen mara baada ya kutangazwa mshindi katika shindano hilo usiku huu
Warembo wa Redds Miss World Tanzania wakicheza shoo ya ufunguzi
Mkurugenzi wa kamati ya Miss Tanzania Hashim Lundenga akijichanganya na wageni waalikwa katika shindano hilo.
Baadhi ya Majaji wa shindano hilo wakijadili jambo kutoka kulia ni Mshauri wa kamati ya Miss Tanzania Ramesh Shah, Miriam Ikoa na Prashant Patel Mwenyekiti wa kamati ya Miss Tanzania. Chanzo:- http://www.fullshangweblog.com
Warembo hao wakipta jukwaani na vazi la jioni
Wakionyesha Shoo yao ya ufunguzi.
Mrembo Hamisa Hassan akipita na vazi la ubunifu
M rembo Pendo Laizer akipita na vazi la ubunifu
Mshauri wa kamati ya Miss Tanzania Ramesh Shah akitangaza warembo walioingia katika tano bora
 Mwenyekiti wa kamati ya Miss Tanzania Prashant Patel akimtangaza Lisa Jensen wa tatu kutoka kulia kama mshindi wa shindano hilo mara baada ya kuwashinda wenzake tisa alioingia nao katika shindano hilo 
  

Post a Comment

Previous Post Next Post