Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akisalimiana na
Mkurugenzi wa Kampuni zinayotowa Mafunzo ya Uzamiaji na Uokozi za Nchini
Uingereza. Mazungumzo yao yalifanyika nyumbani kwa Balozi Seif Mazizini
Nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.
Mkurugenzi
wa Kampuni zinazotowa mafunzo ya upigaji mbizi na Uokozi { L&W na
In Deep Diver Training } za Nchini Uingereza Bw. Jim Kellett akizungumza
na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi nyumbani
kwake mazizini Nje kidogo ya Mji wa Zanzibar. Bw. Jim na Timu yake yuko
Nchini kuendesha mafunzo ya Wiki mbili ya uzamiaji na uokozi kwa Kikosi
Maalum cha Kuzuia Magendo KMKM.
Mabingwa
wa Kampuni inayojishughulisha na masuala ya Mafunzo ya upigaji mbizi na
Uokozi ya Nchini Uingereza { In Deep Diver Training } na kampuni ya
L&W inakusudia kuendeleza mafunzo ya uzamiaji kwa Vijana wa Taasisi
tofauti za Zanzibar baadaye Mwezi wa Novemba mwaka huu wa 2012.
Mkurugenzi
Mkuu wa Kampuni hizo Bw. Jim Kellett amesema mafunzo hayo
yatawashirikisha Vijana 30 kutoka Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo KMKM,
Shirika la Uvuvi wakiwemo pia wawakilishi wa Taasisi za Utalii.
Mkurugenzi
huyo wa Kampuni ya Mafunzo na Huduma za upigaji mbizi alifahamisha
kwamba Taasisi yake imeamua kuendesha Mafunzo kama hayo katika Nchi
mbali mbali kwa lengo la kuwajengea uwezo Vijana wa kutumia Vipaji vyao
katika Biashara ya upigaji mbizi.
Amesema
mbali ya fani hiyo kutumiwa katika masuala ya uokozi lakini pia
itasaidia kutoa ajira kwa Vijana waliomo ndani ya Sekta ya Utalii.
Bw. Jim ameelezea kufurahishwa kwake na mazingira mazuri aliyoyashuhudia Zanzibar katika nyanja ya uzamiaji.
Aidha
ameishauri Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuzipitia Sheria na Kanuni
za Uokozi kwa lengo la kuzifanyia marekebisho ili ziende na wakati wa
sasa.
Naye
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi aliupongeza
uongozi wa Kampuni zote mbili chini ya Mkurugenzi wao kwa uamuzi wao wa
kutoa Mafunzo ya Wiki mbili kwa Askari 30 wa Kikosi Maalum cha Kuzuia
Magendo Zanzibar { KMKM }.
إرسال تعليق