Andre Villas-Boas aanza kazi kwa kumsajili kiungo mshambuliaji wa Brazil

Andre Villas-BoasKOCHA Andre Villas-Boas anataka aanze kazi Tottenham kwa kumsajili kiungo mshambuliaji wa Brazil, Oscar kutoka Internacional. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20 anapatikana kwa dau la pauni Milioni 20.


Wakati huo huo klabu ya Tottenham iko tayari kumsaidia kocha wake mpya, Andre Villas-Boas katika soko la usajili kwa kumkatia pauni Milioni 50. Kocha Mreno huyo anataka kuwasajili mshambuliaji wa Marseille, Loic Remy, beki wa Ajax na Ubelgiji, Jan Vertonghen, kiungo wa Hoffenheim, Gylfi Sigurdsson, kiungo wa CSKA Moscow na Urusi, Alan Dzagoev na kipa wa Birmingham, Jack Butland watue White Hart Lane.

Post a Comment

أحدث أقدم