Na Editha Majura
http://www.mwananchi.co.tz/
TUKIO la Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Adam Malima kutuliza mzuka wa Mbunge wa Viti Maalum, Al-Shaymaa Kwegyir aliyeangua kilio limeacha simulizi.
TUKIO la Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Adam Malima kutuliza mzuka wa Mbunge wa Viti Maalum, Al-Shaymaa Kwegyir aliyeangua kilio limeacha simulizi.
Si kawaida ukumbi wa Bunge la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania mjini Dodoma kushuhudia vilio, lakini kwanini
Mbunge Al-Shaymaa Kwegyir (CCM) aliangua kilio?
Huku akivuta hatua kutoka nje ya ukumbi wa bunge, mbunge huyo aliendelea kulia na kufuta machozi aliyoshindwa kuyazuia.
Kisa?
Ni baada ya kushindwa kustahimili mzigo wa uchungu alioubeba moyoni
mwake, kufuatia ukatili na mauaji dhidi ya wenye ulemavu wa ngozi,
(albino) yanayoendelea nchini huku kasi ya wanaohusika na matukio hayo
kutiwa mbaroni ili wahukumiwe kwa mujibu wa sheria ikisuasua.
Kwa
tukio hilo, Kwegyir ambaye pia ni mlemavu wa ngozi amewaambukiza
Watanzania wenye utu simanzi ikitarajiwa kuonekana mabadiliko katika
namna ya kudhibiti mauaji hayo kwa kuwepo ongezeko la wanaohusika
kufichuliwa na kutiwa nguvuni.
Mfano halisi wa mateso wanayopata
walemavu hao nchini ni maisha ya ukimbizi wanayoishi Omari Mketo na
Joseph Mketo (21) wazaliwa wa baba na mama mmoja.
Ni wazaliwa wa
Kilwa Kipatimu mkoani Lindi, lakini kwa sasa wanaishi Dar es Salaam eneo
la Mtoni Kijichi walikohamia wakitokea Kanda ya Ziwa, Mwanza ambako
alikwenda baada ya baba yao kumwacha mama yao kwa sababu alizaa kwa
mfululizo watoto watano wenye ulemavu huo.
“Tumezaliwa saba,
watano tukiwa wenye ulemavu wa ngozi, lakini mmoja wetu alifariki
tumebaki wanne, wawili wa kike na sisi ni wa kiume,” anaeeleza Omari
anaeleza na kisha kuendelea:
“Mtoto wa kwanza na wa pili hawana
ulemavu huu, lakini kuanzia wa tatu mpaka wa saba ambaye ni Joseph
aliyezaliwa mwaka 1991 tuna ulemavu na ndiyo sababu mwaka 1996 baba
alimwacha mama, nasi tukalazimika kwenda kuishi naye naye nyumbani kwao
Mwanza.”
Joseph anasema, kutokana na ugumu wa maisha pamoja na
hofu kwamba hata baba yao anaweza kuwasaliti kwa sababu haikuwa na
kificho kwamba aliwachukia, waliamua kutorokea Kanda ya Ziwa mkoani
Mwanza huku wakimwachia mama yao huzuni isiyoelezeka.
Anasema
wanashukuru Mungu, dada zao wenye ulemavu wameolewa mmoja anaishi
Mbagala na mwingine Chanika, “sisi bado tunaishi kwa kuhamahama
tukihofia kuuawa huku tubuni na kutekeleza majukumu yanayotuwezesha
kupata mahitaji muhimu katika maisha yetu ya kila siku.”
Wakiwa
Kanda ya Ziwa, Joseph anasema walinunua ndizi sehemu mbalimbali mkoani
Kagera na kuzisafirisha mpaka Mwanza ambapo waliziuza.
Anasema
kazi hiyo iliwawezesha kujipatia mahitaji yao ya kila siku ikiwamo dawa
wanazotumia kuzuia magonjwa mbalimbali yanayowaandama kutokana na
ulemavu wao, hususan magonjwa ya ngozi.
Mtoto wa baba yao mdogo,
Salumu Mzome ambaye pia ni mlemavu wa ngozi aliungana nao mkoani Mwanza
ambako kutokana na biashara waliyokuwa wakifanya maisha yalikuwa mazuri.
Hata
hivyo, walilazimika kuendeleza utaratibu wa kuhamisha makazi ambapo
sasa yapata miezi Minane tangu walipohamishia makazi yao jijini Dar es
Salaam, Mtoni Kijichi.
“Ingawa hatujakumbwa na jaribio la kuuawa
matukio alinayotokea mara kwa mara Tarime, Tabora, Shinyanga na maneno
ya watu kila walipotuona kama vile ‘dili hizo’ tukaona umuhimu wa
kuhamisha makazi,” Joseph anabainisha
Kutokana na Dar es Salaam kuwapo Juakali, wanashindwa kufanya kazi ambazo hufanywa na watu wengi wenye kipato cha chini ili kujikimu kimaisha, kwa sababu ya kuepuka miale ya Jua ambayo huathiri ngozi na hatimaye kuugua ugonjwa wa saratani.
Kutokana na Dar es Salaam kuwapo Juakali, wanashindwa kufanya kazi ambazo hufanywa na watu wengi wenye kipato cha chini ili kujikimu kimaisha, kwa sababu ya kuepuka miale ya Jua ambayo huathiri ngozi na hatimaye kuugua ugonjwa wa saratani.
Wamebuni mradi wa intaneti ambamo pia watauza vifaa
mbalimbali vya ofisini na shuleni (stationery) wakiamini kuwa
wakifanikiwa katika hilo, watamudu kujipatia mahitaji yao muhimu katika
maisha yao ya kila siku na ngozi zao kubaki salama bila hatari ya
saratani.
Ili wafanikiwe katika hilo, vijana hao wanahitaji
ufadhili kutoka kwa watu binafsi, taasisi binafsi, za serikali, za
kidini na mashirika ya umma. Mahitaji wanayoainisha kuwa ni muhimu
katika kufanikisha mpango huo ni Sh 5,150,000 (milioni tano na laki moja
na nusu)
Wanahitaji kompyuta nne zinazogharimu Sh 1,400,000,
mashine ya kurudufia, Sh 1,000,000, mashine ya lamination Sh 100,000 na
gharama za uendeshaji Sh 1,000,000 Pango, Sh 720,000, feni Sh 150, 000
Meza mbili Sh 400,000, Viti vya plastiki Sh 60,000 mashine ya binding
Sh. 120,000 na printer ya Sh 200,000
Wao wana matumaini makubwa
kwamba, Watanzania wengi wenye imani na wanaoguswa na hali ngumu ya
maisha ikiwamo ya kiusalama inayowakabili, watajitolea kuwawezesha
kufanikisha mpango wao huo ambao pamoja na kwamba utawasaidia pia utatoa
mwanya kwa baadhi ya vijana wasiokuwa walemavu kupata ajira.
Wanamwomba
yeyote mwenye nia ya kuwachangia kwa kiwango chochote, kuwasilisha
mchango wake kwa kupitia katika Akaunti yenye nambari 054206006477 NBC
au kupitia ofisi za gazeti la Mwananchi, Tabata Relini.
إرسال تعليق