URA YATINGA ROBO FAINALI KAGAME

URA YATINGA ROBO FAINALI KAGAME,

Wachezaji wa URA wakishangilia bao la tatu

URA ya Uganda, imekuwa timu ya kwanza kufuzu Robo Fainali ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame kutoka Kundi A, baada ya kuichapa mabao 3 -1, AS Vita ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam jioni hii.
Mabao ya URA yaliwekwa wavuni na Sula Bagala (mawili) na Robert Ssentongo, wakati la kufutia machozi la Vita, inayofundishwa na kocha wa zamani wa Yanga, Raul Jean Pierre Shungu lilifungwa na Mutombo Kazadi.
URA sasa imefikisha pointi sita baada ya kucheza mechi mbili na kushinda zote na itamaliza na Ports ya Sudan kutafuta kujihakikishia uongozi wa kundi hilo tu.

Post a Comment

أحدث أقدم