ULAYA LEO NA MAGAZETI YAO, SOMA MANCIN ANAVYOLONGA, FERGUSON KUNANI? PERUZI

MAN CITY WALITOA OFA KWA MESSI, IKAPIGWA CHINI...

Adam Johnson
Adam Johnson
Kitabu kipya kinasema kwamba, Manchester City "kwa bahati mbaya" ilitoa ofa ya kumsajili Lionel Messi, lakini kiulaini ikakataliwa, katika usiku ambao klabu hiyo ilichukuliwa rasmi na Sheikh Mansour mwaka 2008.
 

FERGUSON AMEBAKIZA MIAKA MIWILI 

Sir Alex Ferguson anataka kustaafu ndani ya miaka miwili, baada ya kutengeneza timu mpya, inayoongozwa na Wayne Rooney na Robin van Persie.
Habari kamili: Mail on Sunday
 
 
Roberto Mancini haridhiswhi na usajili wa pauni Milioni 12 wa Jack Rodwell kutoka Everton na bado anashangazwa na usajili wa Man City safari hii.
Habari kamili: Mail on Sunda
 

MODRIC AIKATAA TENA CHELSEA, YEYE NA REAL MADRID TU

Luka Modric, mwenye umri wa miaka 26, anajiandaa kuipiga chini ofa mpya ya Chelsea na kuhamia Real Madrid wiki hii.
 Habari kamili: Sunday Mirror
 
 
Adam Johnson anajiandaa kuondoka Man City na kurudi nyumbani kwao, Kaskazini Mashariki, na Sunderland iko tayari kutoa pauni Milioni 10kwa ajili ya winga huyo wa England.
Habari kamili: Sun on Sunday

Post a Comment

Previous Post Next Post