Cesc Fabregas akionyesha sura yake isiyo na furaha |
Cesc Fabregas ameelezea kuchanganyikiwa kwake juu ya namna anavyotumika kwa sasa Barcelona.
Kiungo
huyo wa kimataifa wa Hispania, ambaye ameelezea kuchanganyikiwa kwake
na kuchezeshwa sehemu tu tu mchezo, alitolewa dakika ya 63 katika
ushindi mwembamba wa Barca dhidi ya Valencia Jumapili.
Licha
ya kuanza kwenye mechi zote tatu za La Liga msimu huu, Fabregas anabaki
asiye na furaha katika klabu iliyomuibua kisoka na kumkuza kabla ya
kuuzwa Arsenal, na kurejea Nou Camp msimu uliopita kwa dau la pauni
Milioni 30 baada ya miaka nane ya kuishi London.
Hivi
karibuni mshambuliaji wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo, naye aligoma
kushangilia mabao yake dhidi ya Granada kutokana na kutofurahia maisha
Santiago Bernabeu
Machungu ya Cristiano Ronaldo hayafichiki Real Madrid
"Kila mmoja anapenda kucheza dakika zote za msimu. Nimekuwa nikisema wakati wote nachezea timu bora duniani, lakini nimekuja hapa kushindana, kujifunza na kufurahia, siyo kuumiza kichwa changu.
"Kocha
anajua uwezo wangu. Lakini katika nafasi zote tatu ninazoweza kucheza,
nashindana na wachezaji watatu bora duniani. Nafurahi kuwa sehemu ya
timu hii, lakini kocha akiniambia natakiwa kuondoka, nitaondoka.
"Lakini
sitampa wepesi wa kufanya hivyo, kwa namna yoyote. nitaendelea,
kuangalia mbele hadi mambo yabadilike. nimekuja hapa kufanya kazi kwa
ufanisi,"alisema Fabregas.
Zaidi soma: http://www.dailymail.co.uk
Post a Comment