Makamu
 wa chuo cha VETA mkoani Singida,akizungumza muda mfupi kabla ya 
kufunguliwa kwa mkutano wa madereva wa magari ya abiria mkoani Singida.
Kaimu
 mkurugenzi mkuu wa SUMATRA Bw. Ahmad Kilima akizungumza kwenye hafla ya
 kufungua mkutano wa madereva wa magari ya abiria mkoani Singida.Mkutano
 huo uliofanikiwa ulifanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa chuo cha VETA 
mjini Singida.Kushoto ni kamanda wa polisi mkoa wa Singida Linus 
Sinzumwa.
Mkuu
 wa kikosi cha usalama barabarani mkoani Singida, Mohammed Likwata 
akitoa taarifa yake kwenye mkutano wa madereva wa magari ya abiria 
ulioitishwa na SUMATRA.
Baadhi
 ya madereva wa magari ya abiria waliohudhuria mkutano ulioitishwa kwa 
ajili yao na SUMATRA.(Picha zote na Nathaniel Limu).
Madereva
 nchini wamehimizwa kuanzisha vyama vyao ili kujijengea mazingira mazuri
 ya kuweza kukabiliana kisayansi na changamoto zinazowakabili ikiwemo ya
 kulipwa maslahi duni na waajiri wao.
Wito
 huo umetolewa na kaimu mkurugenzi mkuu wa SUMATRA,Ahmad Kilima wakati 
akizungumza kwenye ufunguzi wa mkutano wa madereva wa magari ya abiria 
mkoani Singida.
Alitaja
 changamoto zingine zinazowakabili madereva,kuwa ni kutokuwa na ajira za
 uhakika na uwezo mdogo wa kujisomesha au kujiendelea kielimu,ili kuwa 
na ufahamu mkubwa wa sheria na kanuni za usalama barabarani.
Kaimu
 meneja huyo alisema SUMATRA inaamini kuwa wamiliki wa mabasi na  malori
 au waendeshaji  wa makampuni ya mabasi na malori na madereva 
wenyewe,kwa pamoja wanayo nafasi kubwa ya kuchangia kupunguza ajali 
nchini.




Post a Comment