
Hamdu
 zote ni za Allah, Mola Mlezi wa viumbe pia. Na rehema za Allah na 
salamu Zake zimfikie Mtume Mtukufu Mwaminifu na Aali zake watoharifu, 
wateule na masahaba wake wema.
Msimu
 wa Hija uliojaa rehema na baraka umewadia na kwa mara nyingine na watu 
waliofanikiwa kwenda katika miadi hii iliyojaa nuru, wamo katika 
kumiminiwa baraka za Mwenyezi Mungu. Hapa, ninatoa mwito kwenu nyote 
mahujaji kutumia fursa ya kuwepo mahala hapa na kuwemo katika wakati 
huu, kujiimarisha kimaanawi na kimaada. Hapa, Waislamu wanaume kwa 
wanawake wanaitikia labeka mlingano wa Mola wao Mkubwa wa kujipamba kwa 
sifa na matendo mema; kwa nyoyo na midomo yao.
Hapa
 watu wote wanapata fursa ya kufanya mazoezi ya kudumisha udugu, 
mshikamano na kujiepusha na maasi. Hii ni kambi ya malezi na mafunzo, ni
 maonyesho ya umoja, adhama na jinsi umma wa Uislamu ulivyokusanya 
pamoja sura za watu tofauti, ni kambi ya kupambana na shetani na 
mataghuti. Hapa Mwenyezi Mungu Mwingi wa hekima na Muweza amepafanya 
kuwa ni mahala ambapo waumini waweze kuona manufaa yao ndani yake. 
Tutakapofungua macho yetu ya busara na ibra basi ahadi ya mbinguni 
itaweza kuenea katika maisha yetu yote; ya kila mmoja wetu na ya jamii 
nzima.
Sifa
 za kipekee za amali za Hija ni kule kuchanganya kwake dunia na Akhera 
na kuchanganya kwake masuala ya watu binafsi na ya kijamii. Al Kaaba 
isiyo na doa na iliyotukuka; kutufu miili na nyoyo za watu katika 
mhimili mmoja madhubuti na wa milele; amali ya Sai (baina ya Safa na 
Marwa) na kufanya jitihada za mfululizo na za mpangilio mmoja kutoka 
nukta ya kuanzia hadi nukta ya kuishia; kugura mahujaji wote kuelekea 
kwenye nyuga za ufufuo za Arafa na Mash’ar na shauku na uhudhurishaji wa
 moyo katika Mash’ar na maqam hayo adhimu, huleta unyofu na hali mpya, 
mapambano ya pamoja ya watu wote ya kukabiliana na vielelezo vya 
shetani, na hatimaye kwa pamoja na kutoka kila mahala na kila rangi na 
kila namna; wote wanashiriki kwa pamoja katika amali hizo tukufu 
zilizojaa neema na utukufu na zilizojaa maana na ishara za uongofu. Sifa
 za kipekee za faradhi hii zimejaa maana na madhumuni.
Ni 
amali kama hii ndiyo ambayo inauunganisha moyo na kumkumbuka Mwenyezi 
Mungu, na kuujaza nuru na kuunawirisha upweke wa moyo wa mwanadamu kwa 
imani na taqwa na wakati huo huo kumvua mwanadamu kutokana na mzingiro 
wa ubinafsi na kumsahilishia mambo katika jamii iliyopambika kwa sura za
 kila namna, ya umma wa Kiislamu na kumvisha nguo ya kujiepusha na 
madhambi ambayo huilinda roho yake kutokana na mashambulizi yaliyojaa 
sumu ya mashambulizi na vile vile humuongezea nguvu na moyo wa kupambana
 na mashetani na mataghuti. Ni mahala hapo ndipo ambapo hujaji anapoweza
 kuonana na Waislamu wenzake wengi wanaunda umma mkubwa wa Kiislamu na 
kuona kwa karibu nguvu na uwezo wa umma huo na hivyo kupata matumaini 
kuhusu mustakbali mwema na vile vile kupata hisia za wajibu wa kutoa 
mchango wake wa kuimarisha umma huo na pia kama atapata taufiki na 
msaada wa Mwenyezi Mungu aweze kutoa bay’a na kutangaza utiifu wake kwa 
Mtume (Muhammad) Mtukufu wa daraja na kufunga mithaki na ahadi imara kwa
 Uislamu azizi na kutia nia ya kweli ya kuijenga kiimani nafsi yake, 
kuleta marekebisho katika umma na kutia nguvu neno la Uislamu.
Mambo
 yote haya mawili, yaani kuijenga nafsi na kuujenga umma (wa Kiislamu) 
ni faradhi zisizoishiwa na wakati na wala zisizofungwa. Njia za kuweza 
kufanikisha faradhi hizo mbili si nzito kwa watu wenye mazingatio na 
wanaoangalia mambo kwa kina katika utekelezaji wa majukumu ya kidini na 
kutumia vizuri akili, tabasuri na wenye mtazamo wa mbali.
Kujenga
 nafsi huanzia kwenye kupambana na hisia za kishetani na kufanya juhudi 
za kujiepusha na madhambi na kujenga umma huingia sura kwa kumjua adui 
na njama zake, kufanya jitihada za kupelekea mashambulizi, hadaa na 
uadui wa maadui usiwe na athari zozote na hadi kufikia kwenye 
kuziunganisha nyoyo na mikono pamoja na lugha za matabaka yote ya 
Waislamu na mataifa yote ya Kiislamu.
Katika
 wakati huu tulio nao hivi sasa, moja ya masuala muhimu zaidi ya umma wa
 Kiislamu ambalo lina mfungamano (wa moja kwa moja) na mustakbali wa 
umma wa Kiislamu, ni matukio ya mapinduzi katika nchi za kaskazini mwa 
Afrika na katika eneo la Mashariki ya Kati ambayo hadi sasa 
yameshapelekea kuanguka tawala kadhaa fasidi na vibaraka wa Marekani na 
waitifaki za Uzayuni na kuzitikisa tawala nyingine kama hizo. Kama 
Waislamu watapoteza fursa hii adhimu na iwapo watashindwa kutumia fursa 
hii katika kuujenga vizuri na kuleta marekebisho kwenye umma wa 
Kiislamu, basi watakuwa wamepata hasara kubwa. Hivi sasa mabeberu 
wavamizi na waingiliaji wa masuala ya ndani ya mataifa mengine wanafanya
 juhudi zao zote kujaribu kupotosha harakati hizo adhimu za Kiislamu.
Katika
 harakati hizo kubwa, Waislamu wake kwa waume wamesimama kupambana na 
ukandamizaji wa watawala (wao madhalimu) na kupambana na udhibiti wa 
Marekani ambao umepelekea kudhalilishwa na kudunishwa mataifa ya 
Waislamu na kusababisha kushuhudiwa ushirikiano baina ya tawala za nchi 
hizo na utawala mtenda jinai wa Kizayuni. Waislamu wamegundua kuwa kitu 
kinachoweza kuwaokoa katika mapambano haya ya kufa na kupona ni Uislamu,
 mafundisho ya dini hiyo tukufu na nara na kaulimbiu zake zenye uwokovu 
na hilo wamelitangaza wazi wazi. Ajenda yao kuu wameifanya kuwa ni 
kulitetea taifa madhulumu la Palestina na kupambana na utawala ghasibu 
(wa Kizayuni). Wamenyoosha mkono wa urafiki kwa mataifa yote ya Waislamu
 na wanataka kuona umma wa Kiislamu unashikamana na kuwa kitu kimoja.
Hii 
ndiyo misingi mikuu ya harakati za wananchi kwenye nchi ambazo katika 
kipindi cha miaka miwili iliyopita, wananchi wake wamenyanyua bendera ya
 uhuru na mabadiliko na kujitokeza kwa viwiliwili na roho zao kwenye 
medani za mapinduzi na ni mambo kama haya ndiyo yanayoweza kuwa misingi 
mikuu ya kuleta marekebisho katika umma mkubwa wa Kiislamu. Kusimama 
imara na kushikamana vilivyo na misingi mikuu ni sharti la lazima la 
kuweza kupata ushindi wa mwisho wa harakati za wananchi kwenye nchi 
hizo.
Lengo
 la adui ni kutaka kuhakikisha anateteresha misingi hii mikuu. Mikono 
fasidi ya Marekani na NATO na Uzayuni inatumia baadhi ya mighafala na 
mitazamo finyu kujaribu kupotosha wimbi la harakati ya vijana Waislamu 
na wanatumia jina la Uislamu kuwagombanisha Waislamu na wanaiita jihadi 
ya kupambana na ukoloni na Uzayuni kuwa ni ugaidi usio na macho katika 
ulimwengu wa Kiislamu ili Waislamu wauane wao kwa wao na hivyo maadui 
hao wa Uislamu waweze kuokoka na Uislamu na wanajihadi wake watazamwe 
kwa sura mbaya na chafu.
Baada
 ya maadui kukata tamaa kwa kuona kuwa hawawezi kuushinda Uislamu wala 
kuzima nara na kaulimbiu zake, hivi sasa wameamua kuzusha fitna kati ya 
makundi tofauti ya Waislamu na wanafanya njama za kueneza chuki dhidi ya
 Ushia na chuki dhidi ya Usuni ili kuzuia kupatikana mshikamano na umoja
 katika umma wa Kiislamu.
Maadui
 wanawatumia vibaraka wao katika eneo (la Mashariki ya Kati), kuzusha 
mgogoro nchini Syria ili kuzishughulisha akili za mataifa ya dunia na 
kuzifanya zisahau masuala muhimu ya nchi zao na zisahau pia hatari 
zinazowakabili. Maadui hao wanajaribu kuwashughulisha (Waislamu) na 
masuala ya umwagaji wa damu ambayo maadui wameyazusha wao wenyewe. Vita 
vya ndani nchini Syria na kuuliwa vijana wa Kiislamu kwa mikono ya 
Waislamu wenzao ni jinai ambazo zilianzishwa na Marekani na Uzayuni na 
tawala tiifu kwa maadui ambazo wanazidi kuchochea moto huo. Nani anaweza
 kuamini kuwa, tawala ambazo zilikuwa waungaji mkono wa madikteta waovu 
wa Misri na Tunisia na Libya, hivi sasa wamekuwa waungaji mkono wa 
kutaka demokrasia taifa la Syria? Kadhia ya Syria ni suala la kulipiza 
kisasi dhidi ya utawala wa nchi hiyo ambao katika kipindi cha miongo 
mitatu ulikuwa umesimama peke yake kupambana na Wazayuni maghasibu na 
kuyaunga mkono makundi ya wanamuqawama wa Palestina na Lebanon.
Sisi
 tunaliunga mkono taifa la Syria na tunapinga uchochezi na uingiliaji wa
 aina yoyote ile wa kigeni nchini humo. Marekebisho ya aina yoyote ile 
nchini humo inabidi yafanywe na wananchi wenyewe na kwa kutumia njia 
zinazokubaliwa kikamilifu na wananchi wa taifa hilo. Hatua ya mabeberu 
wa kimataifa ambao kwa msaada wa tawala za vibaraka wao katika eneo hili
 wanatumia kisingizio cha kuenea mgogoro na wakati huo huo kutumia 
kisingizio cha kuweko mgogoro kuhalalisha kufanya kila aina ya jinai 
nchini humo ni hatari kubwa ambayo kama tawala za eneo hili 
hazitajiepusha nayo basi inabidi zisubiri zamu yao ifike ya kukumbwa na 
hadaa hizo za kibeberu.
Makaka
 na madada! Msimu wa Hija ni fursa ya kutaamali na kuyaangalia kwa kina 
masuala muhimu ya ulimwengu wa Kiislamu. Hatima ya mapinduzi ya eneo 
hili na juhudi za madola makubwa yaliyojeruhiwa kutokana na mapinduzi 
(ya wananchi wa eneo hili) za kutaka kuyapotosha mapinduzi hayo ni 
miongoni mwa masuala hayo (muhimu ya ulimwengu wa Kiislamu ambayo 
inabidi kuyaangalia kwa kina). Njama za wasaliti za kutaka kuzusha 
hitilafu kati ya Waislamu na kuleta ugomvi na suutafahumu kati ya nchi 
ambazo zimeamua kushirikiana na Jamhuri ya Kiislamu; kadhia ya Palestina
 na juhudi za kuifanya itengwe na kuizima jihadi ya Wapalestina; 
propaganda za kueneza chuki dhidi ya Uislamu zinazofanywa na tawala za 
Magharibi na uungaji mkono wa tawala hizo kwa watu wanaomvunjia heshima 
Mtume Muhammad SAW; kuandaa mazingira ya kuzuka vita vya ndani na 
kugawanywa vipande vipande baadhi ya nchi za Waislamu; kuzitisha tawala 
na wananchi wa nchi za Kiislamu zilizofanya mapinduzi kuhusiana na 
hatari za kupinga siasa za kibeberu za Magharibi na kueneza dhana potofu
 kuwa mustakbali wao unategemea kujisalimisha kwao mbele na madola ya 
kibeberu na masuala mengine muhimu sana kama hayo, ni miongoni mwa 
kadhia muhimu ambazo inabidi ziangaliwe kwa taamuli na kwa mazingatio 
makubwa katika fursa inayopatikana kwenye Hija na chini ya kivuli ya 
kupendana na kuwa na fikra moja nyinyi mahujaji.
Ni 
jambo lisilo na shaka kwamba uongofu na msaada wa Mwenyezi Mungu 
utawaangazia njia za salama na amani waumini wenye kufanya jitihada 
katika mambo yao, ?????? ?????? ???? ???????? ?????Na wanaofanya juhudi 
kwa ajili Yetu, Sisi tutawaongoa kwenye njia Zetu. (al Ankabut – 29:69).
Wassalaamu Alaykum Warahmatullahi Wabarakaatuh.
Sayyid Ali Khamenei,
Post a Comment