ELLINAH Wamukoya
ameteuliwa kuwa Askofu wa Kwanza wa Kike wa Kanisa la Kianglikana
barani Afrika. Akiongea muda mfupi baada ya kuteuliwa, Bi. Ellinah
Wamukoya amesema uamuzi huo ni heshima kwa kina mama. Ellinah Wamukoya,
61, sasa atahudumu kama askofu mpya wa kanisa hilo katika ufakme wa
Swaziland, moja wapo ya nchi zinazokisiwa kufuata siasa za kihafidina.
Kutawazwa kwake kumejiri huku Kanisa la Kianglikana, likitarajiwa
kujadili ikiwa kina mama wataruhusiwa kuapishwa kuwa maaskofu wa kanisa
hilo.
Askofu
wa jimbo la Capte Town, nchini Afrika Kusini, amesema kuwa wamechukua
uamuzi huo ili wawe mfano kwa wengine na pia kuwatakia, viongozi wa
kanisa hilo, faraja na hekima ili kujadilia sauala hilo kwa haraka. Kwa
mujibu wa ripoti aliyotuma kwa vyombo vya habari, askofu huyo wa Jimbo
la Cape Town, Revd. Thabo Makgoba, amesema wimbi kwa sasa linavuma na
kuwa wameshuhudia tukio la kihistoria ambao ni sawa na bingu kufunguka.
David
Dinkebogile aliongoza sherehe hizo na kukariri kuwa nia yao kuwa
ilikuwa kumuapisha askofu na wale sio mtu mweusi, muafrika na raia wa
Swaziland. Askofu Wamukoya ni meya wa zamani wa Mji Mkuu wa Swaziland
Manzini.
-BBC/SWAHILI.
Post a Comment