Waziri wa Mawasiliano, Sayansi
na Teknolojia Profesa Makame Mbarawa akizungumza na wageni waalikwa
wakati wa uzinduzi wa mpango kabambe wa Teknohama katika Sekta ya Elimu
nchini uliofadhiliwa na Kampuni ya HUAWEI kutoka China leo.
Katika Mradi huo wa Teknohama
itayowezesha Watanzania mbalimbali kutoka shule za Sekondari na Vyuoni
kupata vifaa na mafunzo ya Sayansi na Teknolojia ili kusukuma mbele
maendeleo katika nyanja za Uchumi na Kijamii.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni
ya HUAWEI kutoka China Bw. Bruce Zhang akizungumza katika hafla hiyo
kwamba Mpango huu unaoitwa "Huawei ICT Star" itasaidia katika shule za
Primary na Sekondari katika kusukuma mbele maendeleo ya Sayansi na
Teknolojia nchini Tanzania.
Alisema katika Program hii
itasaidia kuboresha miundo mbinu katika Sanyansi na Teknolojia ili kutoa
mwamko kwa vijana wa Kitanzania kujifunza masomo ya Sayansi na
Teknolojia.
Balozi wa China nchini Tanzania
Mh. LU YOUQING akitoa maelezo yake wakati wa uzinduzi wa mpango wa
Teknohama katika shule na vyuo nchini Tanzania.
Balozi alisema mpango huu ni
mwendelezo wa uhusiano mwema kati ya Tanzania na Jamhuri ya watu wa
China katika nyanja mbalimbali za biashara uchumi na Kijamii.
Aliongeza kwamba Serikali ya
China itaendelea na mikakati yake ya kusaidia nchi ya Tanzania ili
kuweza kufikia malengo ya Milenia ya 2015.
Meza Kuu.
Mgeni rasmi Mh. Mbarawa na Balozi wa China wakizindua rasmi mpango wa "HUAWEI ICT STAR" nchini Tanzania.
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi
na Teknolojia Profesa Mbarawa na Mkurugenzi Mtendaji wa HUAWEI Bw. Bruce
Zhang wakitiliana saini kitabu cha makubaliano rasmi ya Ushirikiano
katika Sekta ya Sayansi na Teknolojia kupitia Elimu.
Profesa Mbarawa akimkabidhi zawadi kwa Mkurugenzi Mtendaji wa HUAWEI.
Pichani Juu na Chini ni wageni waalikwa waliohudhuria uzinduzi huo.
Mgeni rasmi Waziri Mbarawa akiondoka ukumbi baada ya uzinduzi
! ~~ Huawei Ascend Mate 7 Online Shopping ~~ !
ReplyDeleteHuawei Ascend Mate 7 Price In Dubai | Huawei Ascend Mate 7 Price In Uae
Post a Comment