SIMBA, YANGA JENGENI VIWANJA VYENU.!!

“Yanga na Simba wamekuwa wazungumzaji wazuri kuhusiana na ujenzi wa viwanja, lakini hakuna kinachoonekana,”  hayo ni maneno ya Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo katika Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Juliana Yassoda
Akizungumza Dar es Salaam jana, Yassoda aliwataka kuiga mfano wa klabu changa kama Azam FC ambao ndani ya muda mfupi wameweza kuwa na uwanja , alisema wakati umefika kwa viongozi wa klabu za nchini kufata mfano wa klabu za Ulaya.
Yassoda aliongeza kuwa kwa kufanya hivyo itasaidia kuongeza pato la klabu zao, kuongeza ajira na kupeleka burudani karibu na wadau wao na kuwapa burudani kwa sababu soka ni burudani pia

Post a Comment

أحدث أقدم