Uchumi wa Garissa unateketea kufuatia wimbi la mashambulizi ya karibuni

Jengo la kinu cha Mawa kiliharibiwa wakati wa mapambano baina ya wananchi na vikosi vya usalama hapo tarehe 19 Disemba. Wafanyabiashara wengi mjini bado watalazimika kujenga tangu baada ya tukio. [Bosire Boniface/Sabahi]
Na Bosire Boniface, Garissa

Biashara imeanguka Garissa kufuatia wimbi la mashambulizi ya mauaji mwezi uliopita.


Hashim Ali Abdi, mfanyabiashara wa vipodozi mwenye umri wa miaka 43, alisema kuwa Garissa imekuwa chaguo la wanunuzi madukani kutoka Jimbo la Kaskazini Mashariki kwa muda mrefu sana, lakini mashambulizi ya hivi karibuni yamewafukuza watu.

"Wateja wangu, hasa kutoka Wajir na Mandera, wanasema wanaogopa kuja Garisaa kupata mahitaji yao," aliiambia Sabahi. "Ninawategemea wao kwa kiwango kikubwa."

Mashambulizi yamekuwa yakiongezeka Garissa tangu mwezi uliopita. Al-Shabaab wanahusishwa na shambulizi ambalo liliua maafisa wawili wa polisi tarehe 16 Novemba na jengine lililoua askari watatu tarehe 19 Novemba, ambalo lilifuatiwa na ulipizaji kisasi ambao askari waliwapiga wananchi na kuchoma moto biashara. Tarehe 11 Disemba, polisi iliatia mbaroi watu sita huko Garissa ambao wametuhumiwa kupanga shambulio la kigaidi.

Irene Muthoni, ambaye anamiliki Irene Delicacies Hotel, alisema wateja wamemkimbia kwa sababu ya mashambulizi.

"Wakati wa chakula cha mchana na usiku, hoteli ilikuwa inajaa watu, lakini sasa wateja wamepungua sana," alisema, na kuongeza kuwa ikiwa hali hii itaendelea mwezi huu wa Disemba hadi Januari, basi atalazimika kufunga.

"Ninapoteza pesa," aliiambia Sabahi. "Kila mwezi, nilikuwa ninapata pesa nyingi kuweza kulipia jengo na kuweka akiba kubwa, lakini sasa ninalazimika kutumia akiba kwa kulipia kodi."

Zeinab Sheikh Mohammed, mkurugenzi wa Baraza la Biashara na Viwanda la Kenya katika Jimbo la Kaskazini Mashariki, alisema licha ya vikwzo hivyo, jamii ya wafanyabiashara ina matumaini kuwa hali itarejea kuwa ya kawaida.

"Tunatarajia kuwa zaidi ya shilingi milioni 300 (dola milioni 3.5) katika fursa za biashara zilipotea mwezi Novemba," aliiambia Sabahi, na kuongeza kuwa baadhi ya biashara zilizochomwa moto na askari bado hazijajirudi.

"Tumekuwa na mikutano mingi katika mabaraza ya mji pamoja na maafisa wa usalama ili kutafuta mikakati ya kumaliza vurugu na kila mtu nanawajibika," alisema. "Hakuna mtu aliye salama, kwa vile tulishuhudia wananchi wakivumilia mashambulizi. Hilo linatupa suluhisho la kuimarisha mashirikiano yetu [na polisi] ili kujenga mazingira yanayovutia kwa biashara."

Ushirikiano wa wananchi ni muhimu kwa kushughulikia kwa usalama
Katibu wa Kamati ya usalama ya Garissa Hassan Shurie alisema ni muhimu sana kwa wananchi kushirikiana na vyombo vya usalama ili kuwatambua wahalifu katika jamii.

"Tulipoteza mwanachama mmoja wa kamati ya amani ambaye alipigwa risasi na kuuawa pamoja na askari mmoja wa jeshi la Ulinzi la Kenya tarehe 9 Disemba, lakini tutaendelea kufanyakazi na maafisa wa usalama ili kuwasafisha wahalifu," alisema.

"Wahalifu wanakusudia kujenga chuki za vikundi," alisema. "Mashambulizi haya ni ushahidi kuwa hakuna aliye salama kwa hivyo tunatoa wito wa mashirikiano ili kumaliza vurugu."

Mkuu wa Wilaya ya Garissa Mohamed Maalim alisema mambo yataimarika ikiwa kila mmoja anafanyakazi pamoja.

"Kila mtu ana mengi ya kufanya ili kuimarsha hali hii," aliiambia Sabahi. "Vikosi vya usalama wamefanya wanavyoweza na kuhatarisha maisha yao ili kurejesha amani lakini haliwezi kkufanya hivyo pekee."

Maalim aliwaomba wakazi kushirikiana na serikali katika usajili wa watu unaoendelea ili kuisaidia serikali kusimamia mienendo ya wananchi, moja ya maazimio yaliyofikiwa katika mkutano wa usalama uliofanyika katika baraza la mji mwezi Oktoba.

"Usajili tayari umetayarishwa katika vitongoji vya Waberi, Iftin na Galbet na wale ambao hawakujisajili watachukuliwa kuwa ni wahalifu," alisema.

Sheikh Abdullahi Salat, mwenyekiti wa Baraza Kuu la Waislamu la Kenya huko Garissa, alisema kuwa mashambulizi yataimarisha tu maazimio ya wananchi ili kuhakikisha amani.

"Ufunguo wa kushinda vita hivi ni kuungana pamoja na kufanyakazi kwa karibu na vikosi vya usalama," aliiambia Sabahi. Badala yake, maafisa wa usalama wana jukumu la kuendeleza imani ya wananchi ili kushinda vita dhidi ya al-Shabaab, alisema.

Salat alisema kuwa fujo za tarehe 19 zilizofanywa na askari waliokuwa wanapingwa kuuliwa kwa wenzao watatu, zimemomonyoa imani za wananchi. Hata hivyo, alisema kuwa wakaz bado wanataka kushirikiana.

"Wakazi wameisaidia serikali kupambana na al-Shabaab kwa kujitolea kutoa habari na wataendelea kufanya hivyo," alisema.

Alisema adhabu ya pamoja kwa wakazi kutoka mikononi mwa vikosi vya usalama haipaswi kurejea, na kwamba wanasubiri matokeo ya kamati ya bunge ambayo inachunguza ghasia hizo.

Post a Comment

أحدث أقدم