mwili wa marehemu Mwangosi ukikanywagwa na askari waliokuwa wakimsaidia mwenzao aliyejeruhiwa kwa bomu lililomuua Mwangosi
ASKARI kikosi cha kituliza ghasia (FFU )mwenye namba G2573 Pasificus Cleophace Simoni (23) anayetuhumiwa kumuua aliyekuwa mwandishi wa habari wa kituo cha Chanel Ten mkoani Iringa marehemu Daudi Mwangosi kupandishwa tena kizimbani leo katika mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Iringa.
ASKARI kikosi cha kituliza ghasia (FFU )mwenye namba G2573 Pasificus Cleophace Simoni (23) anayetuhumiwa kumuua aliyekuwa mwandishi wa habari wa kituo cha Chanel Ten mkoani Iringa marehemu Daudi Mwangosi kupandishwa tena kizimbani leo katika mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Iringa.
Mtuhumiwa huyo leo anatarajia kufikishwa tena mahakamani huku tayari mahakama hiyo chini ya hakimu
Dyness Lyimo ikiwa imetoa onyo kwa askari waliomfikisha mahakamani
hapo mara ya mwisho kutokana na kitendo cha kuidharau mahakamani hiyo
kwa kumtoa mtuhumiwa huyo ndani ya chumba cha mahakama kabla ya shughuli
za mahakama kuhitimishwa .
Askari
hao na mtuhumiwa walionyesha kuidharau mahakamani hiyo kwa kumtoa
mtuhumiwa huku mahakama ikiwa inaendelea na kupelekea hakimu kumwagiza
wakili wa serikali kuwafuata askari hao na mtuhumiwa ili kurudi ndani ya
chumba hicho na kuwahoji askari hao kwa kitendo walichokifanya kabla ya
kuomba msamaha .
Kesi hiyo namba namba 1 ya mwaka 2012 ya mauwaji hadi sasa mtuhumiwa huyo amefikishwa mahakamani hapo zaidi ya mara nne na kesi hiyo ikiendelea kutajwa .
Kesi hiyo namba namba 1 ya mwaka 2012 ya mauwaji hadi sasa mtuhumiwa huyo amefikishwa mahakamani hapo zaidi ya mara nne na kesi hiyo ikiendelea kutajwa .
Mtuhumiwa
huyo anatuhumiwa kumuua kwa kwa bomu aliyekuwa
mwandishi wa habari wa Chanel Tena mkoa wa Iringa
marehemu Mwangosi septemba 2 Septemba mwaka jana katika kijiji cha
Nyololo Wilaya ya Mufindi Mkoa wa Iringa wakati wa vurugu kati
ya polisi na wafuasi wa Chadema .kinyume na kifungu cha sheria
namba 148 kifungu kidogo 5A.i cha makosa ya jinai. Kwa mujibu wa kesi za jinai,
sheria kifungu 196 kanuni ya adhabu Cap. 16 iliyofanyiwa marejeo mwaka 2002,
إرسال تعليق