Polisi watoa taarifa kamili za kuzama kwa Jahazi liitwalo Sunrise likitokea Tanga kulekea visiwani Zanzibar

Bahari ya Hindi (Picha ya liblary )
Jioni ya January 31 2013 millardayo.com iliripoti kuhusu kuzama kwa Jahazi liitwalo Sunrise likitokea Tanga kulekea visiwani Zanzibar likiwa na abiria 32 ambapo lilizama kwenye lile eneo la Nungwi .

Polisi Zanzibar walisema “tayari tumeshapokea watu 22 waliookolewa wakiwa wazima na hakuna maiti iliyopatikana mpaka sasa hivi, waliokuwemo kwenye chombo ni watu 32 hivyo watu bado watu 10 hawajulikani walipo”

Baada ya hapo millardayo.com iliahidiwa tena kuongea na Polisi baadae ili kujua zoezi la uokoaji limefikia wapi, kweli Polisi walitoa tamko lao usiku wakati AMPLIFAYA ya CLOUDS FM inamalizika.

Namkariri Kamanda akisema “Oparesheni imemalizika na hakuna yeyote aliepatikana zaidi ya walewale 22 wa mwanzo ambao walipelekwa hospitali na wote wamesharuhusiwa isipokua nahodha ambae bado amelazwa hospitali kwa matibabu, kimsingi shauri linaendelea na upelelezi na baada ya kukamilika sheria itachukua mkondo wake”

Kwa taarifa hiyo inamaana watu 10 ambao hawakuokolewa mwanzoni wanahofiwa kufa maji manake mpaka oparesheni ya uokoaji imemalizika hawakuonekana, kwa ushahidi unaweza kumsikiliza Kamanda wa polisi akiongea hapo chini.

Post a Comment

أحدث أقدم