
.
Hii ni stori nzuri ambayo nimechelewa kuipata lakini nikaona kuna umuhimu wa kuiweka hapa na watu wangu waione.
Mwandishi wa habari Shaffih
Dauda kupitia shaffihdauda.com aliripoti kwamba mchezaji Mbwana Samatta
kasema anaamini goli la ushindi alilofunga dhidi ya Cameroon linatosha
kumsafisha kwa mashabiki zake.
Hiyo imekuja baada ya mashabiki
wa soka kuwazomea pamoja na Thomas Ulimwengu wakati Stars ikicheza na
Zambia mwaka jana kwenye uwanja wa Taifa kutokana na kuchelewa kuripoti
kambini kujiwinda na mchezo huo wa kirafiki.
Kitendo hicho kilimkasirisha
kocha Kim Poulsen ambaye aligoma kuwapanga kwenye kikosi ambacho
kilicheza na Tiafa Stars kuibuka na ushindi wa 1-0 likiwa ni goli la
Mrisho Ngassa kwa shuti la mwendo mrefu.
Mbwana Samatta ambae nyumbani
kwao ni Mbagala Dar es salaam amekaririwa akisema”naamini ushindi huu
utakuwa umewafurahisha mashabiki na kurudisha imani kwetu, haikuwa lengo
kuchelewa kujiunga na kambi, ni mambo tu yaliingiliana”
إرسال تعليق