Uganda yawania nafasi ya urais Mkutano Mkuu Umoja wa Mataifa. imewakilisha
katika Umoja wa Afrika (AU) ugombea wake kwa nafasi ya urais wa Mkutano
Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), nafasi ambayo iwapo itapatikana
itasaidia ushawishi mkubwa katika anga za kimataifa.
Katika
kuwasilisha huko Uganda itakabiliana na maombi kama hayo kutoka
Camoroon ambayo pia imeonyesha nia ya kuwania kiti hicho kwa kikao cha
69 ambacho kitaendeshwa kutoka 2014 hadi 2015.
Akizungumza
na waandishi wa habari, Waziri wa Mambo ya Nje wa Uganda Sam Kutesa
(pichani) amesisitiza kuwa sasa ni wakati wa Afrika kushika wadhfa huo,
tena zaidi Afrika Mashariki.
Amesema
mabara kadhaa yameshika wadhfa huo ikiwemo na sehemu nyingine za Afrika
isipokuwa Afrika Mashariki ambayo ilishika mwaka 1979.
Iwapo
Uganda itafanikiwa, amesema itatumia nafasi yake hiyo kusukuma mbale
suala la kuwemo na nchi ya Afrika katika Baraza La Usalama la Umoja wa
Mataifa.

إرسال تعليق