MH.GODBLESS LEMA APEWA SIKU 7 KUTHIBITISHA KAULI YAKE ALIYOITOA BUNGENI LEO

 
Naibu spika Mh. Job Ndugai amempa siku saba kuanzia leo mbunge wa jimbo la Arusha mjini Godbless Lema kutoa uthibitisho wa kauli aliyoitoa bungeni hii leo kuwa rais jakaya Kikwete ni kinara wa ugaidi hapa nchini

Naibu spika amempa mh. Lema muda huo kufuatia mvutano mkali ulioibuka bungeni wakati akichangia hoja hii leo bungeni Dodoma katika awamu ya pili ya saa 11 jioni

Kufuatia ushauri uliotolewa na Mwanasheria mkuu wa serikali kuwa kauli hiyo iliyotolewa na Lema ni ya kumdhihaki rais, hivyo anatakiwa kuifuta jambo lililokataliwa na Mh. Lema

Kabla ya mh Naibu spika kutoa uamuzi huo mbunge Lema alikubali kuthibitisha kauli yake hiyo ndipo alipopewa siku saba kuanzia leo

Post a Comment

أحدث أقدم