SIMBA YAZIDIWA KETE NA RUVU SHOOTING, YAMNASA CHIPIKIZI COSMAS ADER

            Kikosi cha Ruvu Shooting
KLABU ya soka ya Ruvu Shooting imeizidi kete klabu ya Simba kwa kumsajili mchezaji wa Azam Fc Cosmas Ader aliyekuwa akiicheza kwa mkopo katika klabu ya African Lyon. 
Ader ni mshambuaji chipikizi mwenye kipaji cha hali ya juu alikuwa akiwania pia na klabu ya Simba kabla ya juzi kusaini mkataba wa miaka miwili wa kuichezea Ruvu Shooting. 
Ofisa habari wa Ruvu Shooting Masau Bwire alisema usajili wa mchezaji huo ndio mwanzo wa harakati za kukiimarisha kikosi chao lwa ajili ya msimu ujao wa ligi kuu soka Tanzania Bara. 
Alisema katika kukiimarisha kikosi chao wanatarajiwa kusajili wachezaji watano wapya na kwamba wanafanya usajili wao kimya kimya ili kuepuka kuchezewa rafu zisizo na maana ambazo zimezoeleka katika usajili wa wachezaji hapa nchini. 
“Tunapenda kuutangazia umma wa wapenda soka kwamba Ader kuanzia sasa ni mali ya Ruvu Shooting hivyo klabu yoyote isijusumbue kufanya naye mazungumzo,”alisema 
Ader mwenye kipaji cha aina yake alikuwa ni mmoja ya wachezaji waliowezesha timu ya Vijana ya Azam kutwaa ubingwa wa kombe la Uhai kwa miaka miwili mfululizo 2009 na 2010.

Post a Comment

Previous Post Next Post