SIMULIZI: USILIE NADIA 7

Photo: SIMULIZI: USILIE NADIA
MTUNZI: GEORGE IRON MOSENYA
SIMU: 0655 727325


SEHEMU YA SABA

Fadhaa ile ikanifanya nijikute katika maamuzi ya aina yake, maamuzi ya kurejea Musoma kudai changu….ni lazima nipewe changu…..ama la! Desmund anieleze kwanini aliamua kunitenda vile.
Sikuwa na la kupoteza kwa sasa, nikajikuta napoteza rasmi tabasamu langu, bila shaka roho ya Jadida ilinivamia…..niaamua kurejea Musoma kulisaka jibu la matatizo hayo. Maana haiwezekani yaani nimelawitiwa kisa Desmund, nikabakwa tena na teana kisa yeye, halafu anaendelea kuyafurahia maisha wakati mimi nadhalilishwa hapana Hapana mwandishi, mnyonge mnyongeni lakini haki yake……” Nadia hakuweza kumalizia, akaingia katika kilio cha kwikwi.
“Usilie nadia, nipo kwa ajili yako kama nilivyokwambia sawa!!” nilimweleza kwa sauti ya chini. Kisha nikamvuta na kumkumbatia. Hapa sasa akaanza kulia kwa sauti ya juu kabisa.
Kwa sababu hakuwa akiniona, nami uvumilivu ukanishinda nikajikuta natokwa na chozi hadharani kwa mara ya kwanza tangu nianze kuifuatilia simulizi hii ya Nadia.
******
Usiku ulipita nikiwa chumbani kwangu nikijiuliza, wanaume tumelaaniwa ama? Nilikosa jibu kwa sababu na mimi ni mwanaume kama ni kweli tumelaaniwa basi hata mimi nimelaaniwa pia. 
Nikakosa kundi la kumweka Desmund, nikakosa kundi la kuwaweka wale wanaume waliombaka Nadia akiwa katika hali mbaya kabisa kiafya, nikakosa pia kundi la kumweka Ramadhan Ramso yule mwanaume aliyempa adhabu Nadia ya kufanya mapenzi hadi kupoteza fahamu eti kisa tu alimkatalia ombi lake la kuwa naye katika mahusiano. Kisha baadaye akamkubalia.
“Sasa jamaa yeye ni nani hadi anataka kila anapotongoza akubaliwe?” nilijiuliza. Bado nikakosa jibu, lakini mwisho kwa shingo upande nikakiri kuwa tupo katika kundi moja lakini tabia zilitutenganisha!!!
Hilo lilikuwa wazo langu la mwisho. Nikasinzia!!

****

Nilisikia kama midundo ya ngoma za kizaire, midundo ambayo haikuwa katika mojawapo ya simu zangu. Halafu mbaya zaidi haikuwa katika mpangilio maalum.
Nikajigeuza, kuzikwepa zile kelele, lakini mara zikageuka!! Hazikuwa ngoma za kizaire, bali ulikuwa ni mlango wangu unagongwa!!
Nikasimama wima, nikapekecha macho yangu na kujifunga taulo kiunoni nikajongea mlangoni nikaufungua malango.
Hah! Alikuwa ni Nadia, alikuwa amebadili nguo tayari. Alikuwa ameng’ara na bila shaka alikuwa ametoka kuoga.
“Nchi itauzwa wewe!! Unalala hadi dakika hii, saa tatu sasa.” Alisema huku akionyesha uchangamfu wa hali ya juu. Nikastaajabu, nilikuwa nimelala sana. Nikatabasamu kisha nikainama na kukiri kuwa nilichoka sana usiku uliopita.
Nadia akaaniambia yu chumbani kwake, nikaiufunga mlango nikaoga name nikabadili nguo. Kisha nikamchukua kwa ajili ya kwenda kupata kifungua kinywa!!
Wakati tunakabidhi funguo mapokezi. Yule muhudumu akatuuliza iwapo tulihitaji kufanyiwa usafi ama la!
Mimi nikamwambia sikuwa nahitaji usafi Nadia yeye akamtazama kwa muda bilakusema lolote.
Nikamvuta mkono kando na kumuuliza.
“Nadia,mbona haujamjibu sasa. We unadhani atachukuliaje hapo…sikia Nadia usiruhusu kila mtu ajue matatizo yako sawa.” Nilimkemea. Bado hakunijibu kitu, nikajua tayari kuna jambo limemtokea katika akili yake kama kumbukumbu.
Nikamrudisha chumbani ili asije kusema lolote mbele ya hadhira, na pia kwa upande wangu ilikuwa nafasi nyingine ya kupata majibu ya maswali yangu ama kujua zaidi kuhusu Nadia.
Nikamwingiza chumbani kwangu. Nikategesha vifaa vyangu.
“Mwandishi, sio kwamba nina dharau la! Sio kwamba nilikosa cha kumjibu yule dada hapana! Lakini niliifikiria dunia isiyokuwa na huruma. Dunia mbaya! Dunia inayotunza watu wabaya.
Hivi kweli unaweza kuwa mwanadamu mwenye moyo na damu inayozunguka ukaamua tu kila mara kutumia matatizo ya mtu mwingine kujinufaisha? Halafu mwisho unaheshimika mbele ya hadhira kama mtu mwema?
Sawa nilijipeleka mwenyewe, na nilihitaji sana kuipata nauli ya kwenda Musoma. Sikuwa na raha ndo maana nikaenda pale. Ningekuwa na raha wala nisingeweza kuingia katika kazi hiyo.
Wakati mwingine ni heri ufe katika tatizo moja kuliko kuteseka katika matatizo mbalimbali ambayo kila moja lina uzito mkubwa kuliko lile lililopita.
Duniani kuna matusi na kuna wakutukanwa, ujue mabaamedi tunadharauliwa sana, yaani mwanmaume anakushika makalio anakutukania mama yako lakini ole wako umjibu na achukie!! Eti mmiliki wa baa anadai ni utovu wa nidhamu kumjibu hovyo mteja. Lakini nisingeweza kudhalilisha utu wangu. Nisingeweza hata kidogo kujiuza tena kwa wanaume ninaowachukia.
Mtu unafanikiwa kumtoroka mteja na vishawishi vyake halafu bosi nunayemuheshimu anadiriki kukufanyia ubaya!!
Sikujua kama yule bosi ninayemuheshimu angeweza kunitenda vile, mimi nilijiuona nina msimamo sana na wateja walilifahamu hilo, wewe nitukane nishike matako utakavyo lakini hunipati ng’o, hiyo ndo ilikuwa kauli mbiu yangu.
Nitakufungulia chupa, ukitapika nitadeki ukivunja chupa nitaokota lakini usitegemee nitakunyenyekea katika mwili wangu.
Nilikuwa nimejiwekea kiapo kuwa sitashiriki na wanaume tena, nia yangu kuu ilikuwa kufanikiwa kufikisha nauli ya kwenda Musoma kumkabili Desmund ambaye kuna maswali kadhaa nilitakiwa kupata majibu kutoka kwake. Maana Jadida alivyoenda mara ya kwanza hakupata majibu sahihi, na hata kabla hajajipanga kwenda mara ya pili akabakwa na kuuwawa.

Kutokana na msimamo wangu bosi wangu akanipandisha cheo, nikatokea kuwa baamedi, nikawekwa kaunta. Huku napo nilikuwa makini sana na pia mwepesi katika kuhudumia wateja. Bosi alikuwa akivutiwa na utendaji wangu wa kazi haswaa.
Siku moja bosi alitoa udhuru kuwa anaumwa, na ilikuwa lazima kukabidhi mahesabu jioni, nisingeruhusiwa kulala na pesa ya bosi.
Bosi akapigiwa simu, akampa maelekezo bwana mmoja anipeleke nyumbani kwake kukabidhi zile pesa.

Mimi sikuwa na shaka hata kidogo, nikaamini kuwa bosi alikuwa mgonjwa. Majira ya saa nne huyo bwana akanipeleka nyumbani kwa huyo bosi.
Nilipofika tu sebuleni nilitambua kuwa bosi alikuwa anaishi na familia yake. Picha ukutani zilimwonyesha akiwa na familia, lakini sikusikia hata kelele mle ndani. Bosi akajikongoja kutoka chumbani akiwa na bukta, akaketi huku akijinyoosha viungo nikatoa heshima yangu na kisha kuweka daftari na pesa mezani, tukaanza kupiga mahesabu. Lakini tofauti na siku nyingine bosi wangu alikuwa hana umakini kabisa, nikakiri kuwa bosi alikuwa anaumwa.
Lakini haikuwa hivyo, bosi hakuwa mgonjwa bali ulikuwa mtego tu. Mara akaniomba nimwongoze chumbani kwake akalale kwani kizunguzungu kilikuwa kimemzidia, mimi kama mwanadamu nikafanya alivyoniomba. Nikamshika mkono mmoja na bega nikamkongoja hadi katika chumba chake.
Tulipofika nikadhani atajilaza kitandani lakini badal;a yake akafunga mlango.

“Nadia, ni kweli naumwa…..lakini naumwa ugonjwa wa mapenzi.” Bosi alizungumza huku akionyesha uimara. Nikaduwaa maana sikutegemea jambo hili.

“Hivi Nadia kweli,muda wote huo haujui kama nakupenda. Mimi nimekutoa kwa wale walevi, nimekuweka sehemu yenye pesa, hujui tu kama nakuhitaji, nafasi yako nimewanyikakina Farida, Jeni ambao umewakuta nimekuweka wewe hujajua tu kuwa nakupenda Nadia.” Alinibembeleza huku nikiwa sijielewi bado kama ni ndoto ama vipi? .
Mara akanikumbatia yule mwanaume aliyekuwa ametanuka kifua chake na kitambi kikiwa kinachungulia.

Nilijaribu kujitetea mwandishi, nilimsihi sana lakini hakunielewa hata kidogo. Alikuwa katika matamanio ya hali ya juu.
Nikiwa bado katika kujitetea akanirusha kitandani.
Mwanaume ni mwanaume tu, ana nguvu na akiamua jambo mkiwa wawili hashindwi kamwe!!

Sijui niseme bosi alinibaka la! Hakunibaka, nilikubali yaishe. Maana tulilala naye hadi asubuhi, nikaoga naye huku kila mara nikona aibu kuitazama picha ya mkewe ambayo ni kama ilikuwa ikinitazama nikifanya uchafu na mumewe pale kitandani.

“Sijapenda iwe hivi mama!!! Nisamehe.” Niliiambia ile picha wakati bosi ameenda kuoga.
Aliporejea alikuwa anatabasamu na kuniambia siku inayofuata nisiende kazini, na atatoa taarifa kuwa sitaenda, nilikubali huku nikijiahidi kuwa nitafanya kila niwezalo nipate kiasi fulani cha pesa nyumbani kwa bosi huyo na kisha nitaacha kazi mara moja. Nikiacha kazi nitasafiri kuelekea Musoma kutimiza azma ambayo haikumalizwa na Jadida.
Kilichokuja kutokea majira ya saa sita mchana ndipo kilitokea kituko cha mwaka ambacho kiliyarejesha majonzi lakini kama hiyo haitoshi niliandika historia nyingine.

Bosi alinikuta nikiwa sebuleni nikiwa nimejifunga kanga za mkewe nikiwa natazama luninga huku nikiyafikiria maisha yangu kwa ujumla. Kwa mara ya kwanza nilikuwa nimeketi kwa utulivu katika nyumba kubwa. Nikiwa na mtu ambaye namuamini pia.
Nikiwa kimada rasmi!!
“Nadia!” nilisikia sauti ikiniita kutoka chumbani.
Nikatambua ni bosi, nikaacha kutazama luninga nikakimbilia chumbani.
Nilikutana na macho makali sana yakinitazama, alikuwa ni bosi lakini huyu alikuwa ana hasira sana sikujkua nimemkosea nini ama kuna nini kimetokea, alikuwa na bukta yake.
“Nadia wewe, wewe…..ni wa kuniletea mimi kisonono!!” aliniuliza huku akitetemeka midomo.
Nikastaajabu bila kujua nini cha kujibu.

“Kumbe unapiga umalaya kimya kimya na kujifanya wewe msafi sana. Nadia Malaya wewe…” alishindwa kuendelea akanivamia akanipiga kibao usoni, sijui ilikuwaje lakini kanga ilifunguka nikabaki uchi, akanikamata na kuanza kunichapa na mkanda, nikajitahidi kuomba msamaha lakini hakunielewa. Alinipiga hadi nikatambua kuwa nikiendelea kuvumilia huyu mtu ataniua. Alikuwa ana mkono mzito sana.

Na huu ulikuwa unyanyasaji wa hali ya juu sana, yaani amenilaghai mwenyewe kufanya naye mapenzi, sikuwa na wazo la kuwa na mwanaume. Nikajiweka mbali nao. Sikatai kuwa yawezekana nilimuambukiza huo ugonjwa lakini alinilazimisha mwenyewe kufanya naye mapenzi.
Nilimsihi pia kutumia kinga lakini yeye mwenyewe akanibiashia akalazimisha kila alichotaka kiwe. Kajiambukiza ama nimemwambukiza? Nilijiuliza!!!
Nikapata jawabu kuwa yule mwanaume ananionea.
Ni hapa nilipoukumbuka ukaidi wa Jadida!! Nikayakumbuka mabavu yake aliyokuwa akiwawekea wanaume!
Kwa mara ya kwanza nikaamua kujitetea, lakini katika kujitetea kwangu nikafanya jambo dogo lililozua balaa huku likinihamasisha kufanya zaidi na zaidi.
Nilijikusanya mwili mzima, kisha kwa kichwa kichwa kama kondoo nikamvamia yule mwanaume nikiwa nimeyaunganisha meno yangu. Nikamchota mithili ya ng’ombe nikamtupa mbali.
Kilisikika kishindo mara moja tu na kimya kikatanda!!
Mwandishi nilikuwa sijawahi kuona maiti, hivi kumbe kufa ni sekunde tu, bosi alijibamiza kichwa chake katika marumaru pale ndani.
Kimya kile kilikuwa kimya cha milele!!
Nilitoweka pale nikiwa nimetaharuki, nisijue nini cha kufanya. Nikavaa nguo zangu vyema, nikatoweka pale ndani huku nikiuruka mwili wa yule mwanaume!! 
Hali ilikuwa ya hatari. Hatua kwa hatua hadi nje!!
Nilisikia uzito fulani katika sketi yangu, sikumbuki niliweka nini hapo awali. Nilipojipekua nikakutana n’na kibunda cha pesa. 
Bila shaka yule bosi aliniwekea maksudi kama shukrani kwa penzi nililompa. Na hii ni kabla hajagundua kama nimemwambukiza kisonono. Niliondoka mbio mbio baada ya kutoka nje.
Nilirejea nyumbani kwa Chausiku majira ya usiku sana, huyu ndiye msichana ambaye alikuwa akinihifadhi katika chumba chake huku akiwa anafanya kazi katika baa nyingine jirani na ile niliyokuwa nafanya mimi.
“We Nadia wewe…..umemfanya nini tena bosi wako?” aliniuliza huku akiwa na hofu tele.
“Kwani nini?” nilijifanya sijui lolote.
“Bosi wako si amekutwa amekufa wewe..na wanadai kuna uwezekano kuwa ulilala kwake mwenzangu…mbona kazi sasa.” Alinieleza kwa sauti ya kunong’oneza, kisha akaendelea.
“Nadia mimi dada yako nambie nini kimetokea.” Alinisihi.
“Dada Chausiku mi nimemsukuma tu alitaka kunibaka, kanipiga sasa dada kanipiga kidogo aniue nikajitetea kwa kumsukuma mimi sikuua dada!!!” nilimweleza huku nikiwa nalia.
“Nadia, cha msingi wewe ondoka hapa Mwanza, mimi na wewe ni maskini. Na unafahamu hatuna cha kuwabishia wale wenye pesa, Nadia nilikukuta ukiwa na msiba mzito siku nakuchukua tafadhali sitaki nilie tena ukihukumiwa kwenda jela. Ondoka Nadia ondoka!!!” alinisihi dada yule. Kisha akaingia ndani akatoka na kikopo chake cha kuhifadhia pesa. Akakifungua na kutoa pesa aliyokuwa amehifadhi shilingi elfu ishirini akanipatia.
Nilimtazama, sikuichukua ile pesa nikamkumbatia kwa nguvu, nikahisi upendo mwingine ukitoweka kwangu, nikajipekua katika sketi yangu nikalifungua lile burungutu. Nikatoa noti nne nyekundu nikampatia. Akazikataa na kuniambia kuwa nilikuwa ninayo safari ndefu sana mbele yangu. Akanisihi niende kwa amani…..nililia sana!!
Baada ya siku mbili, Nadia nilikuwa natafutwa kwa kosa la kuua!!
Nikaingia rasmi katika safari nyingine ya maisha ya kikimbizi, yaani ukimbizi katika nchi yangu huru kabisa!!!!
Lakini ningefanya nini iwapo nimelaaniwa!!!
Nina njaa naomba twende kula” alimaliza Nadia….akafuta machozi!!
Nilipata mshtuko kusikia kuwa kumbe Nadia aliwahi kupata kesi ya mauaji!! Laiti angekuwa amemuua Desmund wala nisingeshtuka, kumbe aliua katika jiji ambalo yupo kwa sasa. Mwanza!!! Lakini hakupanga kuua.
Halafu kumbe Jadida aliwahi kwenda Musoma…harakati zipi zilimpeleka dada huyo ambaye ni marehemu tayari.


***NINI KILIJIRI BAADA YA HAPO……..NADIA na kesi ya mauaji!!!
USIKOSE KIPANDE KITAKACHOFUATA
***TOA MAONI YAKO***

SIMULIZI: USILIE NADIA

MTUNZI: GEORGE IRON MOSENYA
SIMU: 0655 727325


SEHEMU YA SABA

Fadhaa ile ikanifanya nijikute katika maamuzi ya aina yake, maamuzi ya kurejea Musoma kudai changu….ni lazima nipewe changu…..ama la! Desmund anieleze kwanini aliamua kunitenda vile.
Sikuwa na la kupoteza kwa sasa, nikajikuta napoteza rasmi tabasamu langu, bila shaka roho ya Jadida ilinivamia…..niaamua kurejea Musoma kulisaka jibu la matatizo hayo. Maana haiwezekani yaani nimelawitiwa kisa Desmund, nikabakwa tena na teana kisa yeye, halafu anaendelea kuyafurahia maisha wakati mimi nadhalilishwa hapana Hapana mwandishi, mnyonge mnyongeni lakini haki yake……” Nadia hakuweza kumalizia, akaingia katika kilio cha kwikwi.
“Usilie nadia, nipo kwa ajili yako kama nilivyokwambia sawa!!” nilimweleza kwa sauti ya chini. Kisha nikamvuta na kumkumbatia. Hapa sasa akaanza kulia kwa sauti ya juu kabisa.
Kwa sababu hakuwa akiniona, nami uvumilivu ukanishinda nikajikuta natokwa na chozi hadharani kwa mara ya kwanza tangu nianze kuifuatilia simulizi hii ya Nadia.
******
Usiku ulipita nikiwa chumbani kwangu nikijiuliza, wanaume tumelaaniwa ama? Nilikosa jibu kwa sababu na mimi ni mwanaume kama ni kweli tumelaaniwa basi hata mimi nimelaaniwa pia. 
Nikakosa kundi la kumweka Desmund, nikakosa kundi la kuwaweka wale wanaume waliombaka Nadia akiwa katika hali mbaya kabisa kiafya, nikakosa pia kundi la kumweka Ramadhan Ramso yule mwanaume aliyempa adhabu Nadia ya kufanya mapenzi hadi kupoteza fahamu eti kisa tu alimkatalia ombi lake la kuwa naye katika mahusiano. Kisha baadaye akamkubalia.
“Sasa jamaa yeye ni nani hadi anataka kila anapotongoza akubaliwe?” nilijiuliza. Bado nikakosa jibu, lakini mwisho kwa shingo upande nikakiri kuwa tupo katika kundi moja lakini tabia zilitutenganisha!!!
Hilo lilikuwa wazo langu la mwisho. Nikasinzia!!

****

Nilisikia kama midundo ya ngoma za kizaire, midundo ambayo haikuwa katika mojawapo ya simu zangu. Halafu mbaya zaidi haikuwa katika mpangilio maalum.
Nikajigeuza, kuzikwepa zile kelele, lakini mara zikageuka!! Hazikuwa ngoma za kizaire, bali ulikuwa ni mlango wangu unagongwa!!
Nikasimama wima, nikapekecha macho yangu na kujifunga taulo kiunoni nikajongea mlangoni nikaufungua malango.
Hah! Alikuwa ni Nadia, alikuwa amebadili nguo tayari. Alikuwa ameng’ara na bila shaka alikuwa ametoka kuoga.
“Nchi itauzwa wewe!! Unalala hadi dakika hii, saa tatu sasa.” Alisema huku akionyesha uchangamfu wa hali ya juu. Nikastaajabu, nilikuwa nimelala sana. Nikatabasamu kisha nikainama na kukiri kuwa nilichoka sana usiku uliopita.
Nadia akaaniambia yu chumbani kwake, nikaiufunga mlango nikaoga name nikabadili nguo. Kisha nikamchukua kwa ajili ya kwenda kupata kifungua kinywa!!
Wakati tunakabidhi funguo mapokezi. Yule muhudumu akatuuliza iwapo tulihitaji kufanyiwa usafi ama la!
Mimi nikamwambia sikuwa nahitaji usafi Nadia yeye akamtazama kwa muda bilakusema lolote.
Nikamvuta mkono kando na kumuuliza.
“Nadia,mbona haujamjibu sasa. We unadhani atachukuliaje hapo…sikia Nadia usiruhusu kila mtu ajue matatizo yako sawa.” Nilimkemea. Bado hakunijibu kitu, nikajua tayari kuna jambo limemtokea katika akili yake kama kumbukumbu.
Nikamrudisha chumbani ili asije kusema lolote mbele ya hadhira, na pia kwa upande wangu ilikuwa nafasi nyingine ya kupata majibu ya maswali yangu ama kujua zaidi kuhusu Nadia.
Nikamwingiza chumbani kwangu. Nikategesha vifaa vyangu.
“Mwandishi, sio kwamba nina dharau la! Sio kwamba nilikosa cha kumjibu yule dada hapana! Lakini niliifikiria dunia isiyokuwa na huruma. Dunia mbaya! Dunia inayotunza watu wabaya.
Hivi kweli unaweza kuwa mwanadamu mwenye moyo na damu inayozunguka ukaamua tu kila mara kutumia matatizo ya mtu mwingine kujinufaisha? Halafu mwisho unaheshimika mbele ya hadhira kama mtu mwema?
Sawa nilijipeleka mwenyewe, na nilihitaji sana kuipata nauli ya kwenda Musoma. Sikuwa na raha ndo maana nikaenda pale. Ningekuwa na raha wala nisingeweza kuingia katika kazi hiyo.
Wakati mwingine ni heri ufe katika tatizo moja kuliko kuteseka katika matatizo mbalimbali ambayo kila moja lina uzito mkubwa kuliko lile lililopita.
Duniani kuna matusi na kuna wakutukanwa, ujue mabaamedi tunadharauliwa sana, yaani mwanmaume anakushika makalio anakutukania mama yako lakini ole wako umjibu na achukie!! Eti mmiliki wa baa anadai ni utovu wa nidhamu kumjibu hovyo mteja. Lakini nisingeweza kudhalilisha utu wangu. Nisingeweza hata kidogo kujiuza tena kwa wanaume ninaowachukia.
Mtu unafanikiwa kumtoroka mteja na vishawishi vyake halafu bosi nunayemuheshimu anadiriki kukufanyia ubaya!!
Sikujua kama yule bosi ninayemuheshimu angeweza kunitenda vile, mimi nilijiuona nina msimamo sana na wateja walilifahamu hilo, wewe nitukane nishike matako utakavyo lakini hunipati ng’o, hiyo ndo ilikuwa kauli mbiu yangu.
Nitakufungulia chupa, ukitapika nitadeki ukivunja chupa nitaokota lakini usitegemee nitakunyenyekea katika mwili wangu.
Nilikuwa nimejiwekea kiapo kuwa sitashiriki na wanaume tena, nia yangu kuu ilikuwa kufanikiwa kufikisha nauli ya kwenda Musoma kumkabili Desmund ambaye kuna maswali kadhaa nilitakiwa kupata majibu kutoka kwake. Maana Jadida alivyoenda mara ya kwanza hakupata majibu sahihi, na hata kabla hajajipanga kwenda mara ya pili akabakwa na kuuwawa.

Kutokana na msimamo wangu bosi wangu akanipandisha cheo, nikatokea kuwa baamedi, nikawekwa kaunta. Huku napo nilikuwa makini sana na pia mwepesi katika kuhudumia wateja. Bosi alikuwa akivutiwa na utendaji wangu wa kazi haswaa.
Siku moja bosi alitoa udhuru kuwa anaumwa, na ilikuwa lazima kukabidhi mahesabu jioni, nisingeruhusiwa kulala na pesa ya bosi.
Bosi akapigiwa simu, akampa maelekezo bwana mmoja anipeleke nyumbani kwake kukabidhi zile pesa.

Mimi sikuwa na shaka hata kidogo, nikaamini kuwa bosi alikuwa mgonjwa. Majira ya saa nne huyo bwana akanipeleka nyumbani kwa huyo bosi.
Nilipofika tu sebuleni nilitambua kuwa bosi alikuwa anaishi na familia yake. Picha ukutani zilimwonyesha akiwa na familia, lakini sikusikia hata kelele mle ndani. Bosi akajikongoja kutoka chumbani akiwa na bukta, akaketi huku akijinyoosha viungo nikatoa heshima yangu na kisha kuweka daftari na pesa mezani, tukaanza kupiga mahesabu. Lakini tofauti na siku nyingine bosi wangu alikuwa hana umakini kabisa, nikakiri kuwa bosi alikuwa anaumwa.
Lakini haikuwa hivyo, bosi hakuwa mgonjwa bali ulikuwa mtego tu. Mara akaniomba nimwongoze chumbani kwake akalale kwani kizunguzungu kilikuwa kimemzidia, mimi kama mwanadamu nikafanya alivyoniomba. Nikamshika mkono mmoja na bega nikamkongoja hadi katika chumba chake.
Tulipofika nikadhani atajilaza kitandani lakini badal;a yake akafunga mlango.

“Nadia, ni kweli naumwa…..lakini naumwa ugonjwa wa mapenzi.” Bosi alizungumza huku akionyesha uimara. Nikaduwaa maana sikutegemea jambo hili.

“Hivi Nadia kweli,muda wote huo haujui kama nakupenda. Mimi nimekutoa kwa wale walevi, nimekuweka sehemu yenye pesa, hujui tu kama nakuhitaji, nafasi yako nimewanyikakina Farida, Jeni ambao umewakuta nimekuweka wewe hujajua tu kuwa nakupenda Nadia.” Alinibembeleza huku nikiwa sijielewi bado kama ni ndoto ama vipi? .
Mara akanikumbatia yule mwanaume aliyekuwa ametanuka kifua chake na kitambi kikiwa kinachungulia.

Nilijaribu kujitetea mwandishi, nilimsihi sana lakini hakunielewa hata kidogo. Alikuwa katika matamanio ya hali ya juu.
Nikiwa bado katika kujitetea akanirusha kitandani.
Mwanaume ni mwanaume tu, ana nguvu na akiamua jambo mkiwa wawili hashindwi kamwe!!

Sijui niseme bosi alinibaka la! Hakunibaka, nilikubali yaishe. Maana tulilala naye hadi asubuhi, nikaoga naye huku kila mara nikona aibu kuitazama picha ya mkewe ambayo ni kama ilikuwa ikinitazama nikifanya uchafu na mumewe pale kitandani.

“Sijapenda iwe hivi mama!!! Nisamehe.” Niliiambia ile picha wakati bosi ameenda kuoga.
Aliporejea alikuwa anatabasamu na kuniambia siku inayofuata nisiende kazini, na atatoa taarifa kuwa sitaenda, nilikubali huku nikijiahidi kuwa nitafanya kila niwezalo nipate kiasi fulani cha pesa nyumbani kwa bosi huyo na kisha nitaacha kazi mara moja. Nikiacha kazi nitasafiri kuelekea Musoma kutimiza azma ambayo haikumalizwa na Jadida.
Kilichokuja kutokea majira ya saa sita mchana ndipo kilitokea kituko cha mwaka ambacho kiliyarejesha majonzi lakini kama hiyo haitoshi niliandika historia nyingine.

Bosi alinikuta nikiwa sebuleni nikiwa nimejifunga kanga za mkewe nikiwa natazama luninga huku nikiyafikiria maisha yangu kwa ujumla. Kwa mara ya kwanza nilikuwa nimeketi kwa utulivu katika nyumba kubwa. Nikiwa na mtu ambaye namuamini pia.
Nikiwa kimada rasmi!!
“Nadia!” nilisikia sauti ikiniita kutoka chumbani.
Nikatambua ni bosi, nikaacha kutazama luninga nikakimbilia chumbani.
Nilikutana na macho makali sana yakinitazama, alikuwa ni bosi lakini huyu alikuwa ana hasira sana sikujkua nimemkosea nini ama kuna nini kimetokea, alikuwa na bukta yake.
“Nadia wewe, wewe…..ni wa kuniletea mimi kisonono!!” aliniuliza huku akitetemeka midomo.
Nikastaajabu bila kujua nini cha kujibu.

“Kumbe unapiga umalaya kimya kimya na kujifanya wewe msafi sana. Nadia Malaya wewe…” alishindwa kuendelea akanivamia akanipiga kibao usoni, sijui ilikuwaje lakini kanga ilifunguka nikabaki uchi, akanikamata na kuanza kunichapa na mkanda, nikajitahidi kuomba msamaha lakini hakunielewa. Alinipiga hadi nikatambua kuwa nikiendelea kuvumilia huyu mtu ataniua. Alikuwa ana mkono mzito sana.

Na huu ulikuwa unyanyasaji wa hali ya juu sana, yaani amenilaghai mwenyewe kufanya naye mapenzi, sikuwa na wazo la kuwa na mwanaume. Nikajiweka mbali nao. Sikatai kuwa yawezekana nilimuambukiza huo ugonjwa lakini alinilazimisha mwenyewe kufanya naye mapenzi.
Nilimsihi pia kutumia kinga lakini yeye mwenyewe akanibiashia akalazimisha kila alichotaka kiwe. Kajiambukiza ama nimemwambukiza? Nilijiuliza!!!
Nikapata jawabu kuwa yule mwanaume ananionea.
Ni hapa nilipoukumbuka ukaidi wa Jadida!! Nikayakumbuka mabavu yake aliyokuwa akiwawekea wanaume!
Kwa mara ya kwanza nikaamua kujitetea, lakini katika kujitetea kwangu nikafanya jambo dogo lililozua balaa huku likinihamasisha kufanya zaidi na zaidi.
Nilijikusanya mwili mzima, kisha kwa kichwa kichwa kama kondoo nikamvamia yule mwanaume nikiwa nimeyaunganisha meno yangu. Nikamchota mithili ya ng’ombe nikamtupa mbali.
Kilisikika kishindo mara moja tu na kimya kikatanda!!
Mwandishi nilikuwa sijawahi kuona maiti, hivi kumbe kufa ni sekunde tu, bosi alijibamiza kichwa chake katika marumaru pale ndani.
Kimya kile kilikuwa kimya cha milele!!
Nilitoweka pale nikiwa nimetaharuki, nisijue nini cha kufanya. Nikavaa nguo zangu vyema, nikatoweka pale ndani huku nikiuruka mwili wa yule mwanaume!! 
Hali ilikuwa ya hatari. Hatua kwa hatua hadi nje!!
Nilisikia uzito fulani katika sketi yangu, sikumbuki niliweka nini hapo awali. Nilipojipekua nikakutana n’na kibunda cha pesa. 
Bila shaka yule bosi aliniwekea maksudi kama shukrani kwa penzi nililompa. Na hii ni kabla hajagundua kama nimemwambukiza kisonono. Niliondoka mbio mbio baada ya kutoka nje.
Nilirejea nyumbani kwa Chausiku majira ya usiku sana, huyu ndiye msichana ambaye alikuwa akinihifadhi katika chumba chake huku akiwa anafanya kazi katika baa nyingine jirani na ile niliyokuwa nafanya mimi.
“We Nadia wewe…..umemfanya nini tena bosi wako?” aliniuliza huku akiwa na hofu tele.
“Kwani nini?” nilijifanya sijui lolote.
“Bosi wako si amekutwa amekufa wewe..na wanadai kuna uwezekano kuwa ulilala kwake mwenzangu…mbona kazi sasa.” Alinieleza kwa sauti ya kunong’oneza, kisha akaendelea.
“Nadia mimi dada yako nambie nini kimetokea.” Alinisihi.
“Dada Chausiku mi nimemsukuma tu alitaka kunibaka, kanipiga sasa dada kanipiga kidogo aniue nikajitetea kwa kumsukuma mimi sikuua dada!!!” nilimweleza huku nikiwa nalia.
“Nadia, cha msingi wewe ondoka hapa Mwanza, mimi na wewe ni maskini. Na unafahamu hatuna cha kuwabishia wale wenye pesa, Nadia nilikukuta ukiwa na msiba mzito siku nakuchukua tafadhali sitaki nilie tena ukihukumiwa kwenda jela. Ondoka Nadia ondoka!!!” alinisihi dada yule. Kisha akaingia ndani akatoka na kikopo chake cha kuhifadhia pesa. Akakifungua na kutoa pesa aliyokuwa amehifadhi shilingi elfu ishirini akanipatia.
Nilimtazama, sikuichukua ile pesa nikamkumbatia kwa nguvu, nikahisi upendo mwingine ukitoweka kwangu, nikajipekua katika sketi yangu nikalifungua lile burungutu. Nikatoa noti nne nyekundu nikampatia. Akazikataa na kuniambia kuwa nilikuwa ninayo safari ndefu sana mbele yangu. Akanisihi niende kwa amani…..nililia sana!!
Baada ya siku mbili, Nadia nilikuwa natafutwa kwa kosa la kuua!!
Nikaingia rasmi katika safari nyingine ya maisha ya kikimbizi, yaani ukimbizi katika nchi yangu huru kabisa!!!!
Lakini ningefanya nini iwapo nimelaaniwa!!!
Nina njaa naomba twende kula” alimaliza Nadia….akafuta machozi!!
Nilipata mshtuko kusikia kuwa kumbe Nadia aliwahi kupata kesi ya mauaji!! Laiti angekuwa amemuua Desmund wala nisingeshtuka, kumbe aliua katika jiji ambalo yupo kwa sasa. Mwanza!!! Lakini hakupanga kuua.
Halafu kumbe Jadida aliwahi kwenda Musoma…harakati zipi zilimpeleka dada huyo ambaye ni marehemu tayari.


***NINI KILIJIRI BAADA YA HAPO……..NADIA na kesi ya mauaji!!!
USIKOSE KIPANDE KITAKACHOFUATA
***TOA MAONI YAKO***

Post a Comment

Previous Post Next Post