Askari
wawili wa wanyamapori (KWS) wameuawa nchini Kenya katika matukio mawili
tofauti ya kukabiliana na uwindaji haramu kwenye hifadhi ya maliasili ya
Kipini iliyoko wilaya ya Tana River nchini humo.
Afisa
uhusiano wa KWS Paul Udoto amesema, jangili mmoja pia ameuawa katika
mapigano hayo, na silaha aina ya AK 47, bunduki 3, na risasi 208
zimekamatwa. Amesema tukio la kwanza lilitokea wakati askari wa
wanyamapori waliokuwa doria kukutana na watu wasiojulikana wanaodhaniwa
kuwa walikuwa wanawinda tembo.
Mapigamo
mengine makali kati ya askari hao na majangili yalizuka saa sita baadaye
na kusababisha kifo cha askari mwingine. Hakuna taarifa zozote kama
kuna majangili waliojeruhiwa katika mapigano hayo.
Chanzo: CRI
إرسال تعليق