Mzee Zahir Ally Zorro kuwaomba 'EX-LOVERS' wake msamaha kupitia Muziki


Mzee Zahir Ally Zoro, Msanii mkongwe wa muziki hapa Bongo ameamua kuwaomba msamaha wanawake wote ambao amekwishakuwa nao katika maisha yake, na wengine kuwapa ahadi kubwa kubwa ikiwepo kuwaoa, ambazo mwisho wa siku hazikutimia. 
Hii ni kupitia ngoma mpya ya Mzee huyu ambayo inakwenda kwa jina Forgive Me, ambayo imefanyika chini ya producer Lamar, kazi ambayo tayari imekamilika na mchakato wa kuisambaza upo mbioni kuanza.
Mzee Zorro amesema wimbo huu unazungumzia historia ya ukweli ya maisha yake ambapo amekiri kuwa amekwishakuwa katika mahusiano mbalimbali ambayo mwisho wa siku hayakuwahi kufika mahali.
Kaa tayari kwa kazi hii ambayo ina ujumbe mzito kwa maisha yao hivi karibuni, ikiwa katika miondoko ya Soul.

Post a Comment

أحدث أقدم