Kiatu cha thamani chamsababisha Lady Jaydee ateleze jukwaani na kuteguka mguu

1234143_10151580358840025_913837710_n
Kama uliangalia Diary of Lady Jaydee wiki iliyopita, ulimshuhudia staa huyo akifanya shopping ya viatu kwaajili ya show yake ya Kili Music Tour jijini Dar es Salaam weekend iliyopita.

Lady Jaydee akiwa backstage na kiatu chake kilichosabisha ateleze jukwaani
Katika show hiyo Lady Jaydee alinunua kiatu cha rangi ya blue, kirefu aka high heels chenye thamani ya shilingi 168,000. Yes laki moja na elfu sitini na nane kama masikio yetu hayakutudanganya.
Hata hivyo urefu wa kiatu hicho ameutaja kuwa chanzo cha kuteleteza jukwaani kwenye show hiyo na kukaribia kumwangusha.
“Kuanguka jukwaani ni ajali kama ajali zingine, isitoshe sikuanguka bali nilikaribia. Ila poleni kwa mlioumizwa na hicho kitendo…Nitapunguza urefu wa viatu siku nyingine,” aliandika jana kwenye ukurasa wake wa Facebook.
“Ni bahati mbaya tu, kwani hata Mwanza/Kahama/Dodoma vilikuwa virefu kama hivyo hivyo na sikuteguka,” alitweet kufafanua kuhusu uvaaji wa viatu virefu jukwaani.

Post a Comment

Previous Post Next Post