Muigizaji wa filamu nchini Blandina Chagula aka Johari yupo
nchini Canada alikoenda kujitambulisha kwa ndugu wa mchumba wake pamoja
na kupanga taratibu za harusi yao.
Akizungumza jana, Irene Uwoya ambaye ni rafiki wa karibu na
Johari amesema kuna mzungu wa nchini Canada aliyetokea kumpenda Johari
nakumtaka kwenda kumtambulisha kwao na kuweka mambo sawa.
“Akitambulishwa kitachofuata ni ndoa,kwa jinsi tulivyojadiliana
watafanya ndoa mbili, moja hapa na nyingine Canada, ili na sisi tulio
Dar es salaam tusheherekee ndoa yake kwasababu kama unavyojua ndugu zake
,marafiki na watanzania kwa ujumla wanahitaji kushuhudia ndoa yao,”
alisema Irene.
“Juzi niliandika kauli ya kumtaka atulie akiwa Canada, sio kwamba
Johari hajatulia ila unajua Johari ni mtu wangu wa karibu,kwahiyo
nilikuwa namwambia abadilike asipeleke uswahili Canada sio kwa nia
mbaya.”
Post a Comment