Hawa ndiyo Wanasoka Mastaa 8 waliopoteza hadhi zao baada ya uhamisho

 
http://static.sportskeeda.com/wp-content/uploads/2012/03/141537883.jpg

Edinson Cavani

UHAMISHO unaofanywa na wanasoka kwa kuhamia klabu zenye upinzani mkubwa, wakati mwingine huwa utata mkubwa katika viwango vyao.
Miongoni mwa uhamisho kama huo ni wa wachezaji Luis Figo, aliyehama kutoka Barcelona na kwenda kujiunga na Real Madrid au Sol Campbell alipohama Tottenham Hotspur na kutimkia Arsenal.
Kwenye Ligi Kuu England, uhamisho wa siku za hivi karibuni uliotingisha ni wa Robin van Persie na Juan Mata, waliozihama klabu zao na kuhamia Manchester United, licha ya kwamba timu zao zina ushindani mkubwa na miamba hiyo ya Old Trafford.
Van Persie alihama kutoka Arsenal na Mata alihama kutoka Chelsea na wote wamejiunga na Man United. Mashabiki wa timu zao za awali,  mara nyingi wamekuwa wakiwaona wachezaji hao kuwa ni wasaliti.
Mbaya zaidi kwa wachezaji wanaofanya uhamisho kama huo, ni kwamba mara nyingi wanakuwa hawaendi kufurahia maisha kwenye timu mpya tofauti na ilivyokuwa kwenye klabu zao za awali.
Kwa mantiki huyo, kuhamia kwenye klabu pinzani siku zote ni kama mchezo wa kamari, huna uhakika wa kwenda kufanya vizuri huku ukifahamika wazi kwamba mashabiki kutoka kwenye timu uliyoihama daima watakuwa wapinzani wako.
Makala hii inawazungumzia wanasoka mastaa ambao wamehama kutoka kwenye timu walizozichezea kwa muda mrefu hadi kujiwekea heshima kubwa na kuhamia timu nyingine na matokeo yake wamekutana na nyakati ngumu tofauti na matarajio yao. Lazima watakuwa wanajutia uamuzi wao.
 
Fowadi huyo wa Uruguay alijengea jina kubwa klabuni Napoli kabla ya kutimkia Paris Saint-Germain. Uhamisho wake ulikuwa wa pesa nyingi hasa kutokana na kiwango cha soka lake alilokuwa akicheza Napoli, lakini tangu alipotua PSG mambo yamekuwa tofauti na matarajio.
Staa huyo kwa siku za hivi karibuni amekuwa hakosekani kwenye vichwa vya habari vya magazeti kila kukicha kwamba anataka kuihama PSG baada ya kuona maisha yamekuwa magumu kwenye Ligi Kuu Ufaransa.
Kitu kimoja kikubwa, alipokuwa Napoli, Cavani alihesabika kama staa wa klabu hiyo, lakini kwenye kikosi cha PSG, amekutana na Zlatan Ibrahimovic ambaye amejenga jina lake katika klabu hiyo ya Paris.
Jambo hilo linakwenda sambamba na Cavani kushindwa kuchezeshwa kwenye nafasi anayotaka ya straika wa kati kwa sababu nafasi hiyo anapewa Ibrahimovic. Cavani alihama kwa ushawishi wa pesa na sasa ametambua kuwa pesa hazina maana tena na ndiyo maana anataka kuhama.
 http://i.telegraph.co.uk/multimedia/archive/02622/stevan-jovetic_2622661b.jpg

Stevan Jovetic


Kwenye timu ya Fiorentina, usingeweza kutaka kikosi cha kwanza cha timu hiyo na kisha ukaliweka kando jina la Stevan Jovetic. Lakini, habari imekuwa tofauti sana baada ya kutua Manchester City. Jovetic alikuwa na furaha sana kwenye maisha yake nchini Italia na hivyo aliondoka kwenye klabu ya Fiorentina mwaka jana na kuhamia Man City akiwa na matumaini ya kwenda kufanya kweli kwenye Ligi Kuu England.

Kwa bahati mbaya kocha, Manuel Pellegrini, amemwona hana jipya na matokeo yake amemfanya kuwa chaguo la nne kwenye safu ya washambuliaji nyuma ya Sergio Aguero, Alvaro Negredo na 

Edin Dzeko.

Kutokana na hilo, Jovetic ameingia kwenye orodha ya wachezaji wanaojutia kuhama kwenye timu ambazo walikuwa wakiabudiwa kama miungo watu na kwenda kwenye timu ambazo wanaonekana kuwa wa kawaida sana.

Kitu pekee anachofurahia staa huyo ni kupokea mshahara mnono, ambao kama mwanasoka amekuwa haufanyii kazi kwa sababu muda mwingi amekuwa akisugua benchi.
 http://www.totaltottenham.com/content/uploads/2013/08/Lamela-spurs.jpg

Erik Lamela


Hayakuwa matarajio kabisa. Erik Lamela wakati anahama AS Roma na kutimkia White Hart Lane, kulikuwa na ahadi nyingi kwamba Tottenham Hotspur ingebadilika na kuwa hatari sana kwenye Ligi Kuu England.

Kwa bahati mbaya, kocha aliyemsajili, Andre Villas-Boas, alitimuliwa. Sasa Lamela ameshindwa kabisa kuonyesha cheche zake alizokuwa akizionyesha kwenye Ligi Kuu Italia.

Staa huyo wa kutoka Argentina, alisajiliwa kwa ada ya Pauni 30 milioni na ameshindwa kuonyesha thamani halisi ya pesa iliyotumika kwenye usajili wake.

Mbaya zaidi amekuwa akisumbuliwa na tatizo la kuwa majeruhi mara kwa mara, kitu kinachomfanya kushindwa kutimiza malengo huku akijiona kuwa uhamisho wake umekuwa mikosi tu, afadhali angebaki AS Roma.
 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhYqTKMsS4o-QTUr3SxJBmasRTHeQJFs5GSENTuEenq9LY5e9yy7EEU6I9_UpeOj_Dk7nsHpfd1neVTdGyUyKSUWueEfaOMFy3GMPhXFD0AW1sIAX9giP015dyPPBl1nVssA1vyWtxHoLM/s1600/2011-08-15_CESC_34.jpg

Cesc Fabregas

 Ni wazi kabisa, Cesc Fabregas, angeonekana kuwa ni mjinga mkubwa kama angegomea nafasi ya kusajiliwa tena na Barcelona mwaka 2011. Nyota huyo alianzia maisha yake ya soka kwenye akademia ya klabu hiyo ya Catalan kabla ya kuhamia Arsenal, ambapo alijenga jina lake na kuwa staa mkubwa wa kikosi hicho ikiwamo kupewa unahodha.
Barcelona ilikuwa kwenye ubora mkubwa duniani, hivyo isingekuwa rahisi kwa mchezaji yeyote kugoma kujiunga nayo kama walikuwa wakimhitaji. Hilo lilimkuta Fabregas na aliamua kutimkia Barcelona na kuupa kisogo umaarufu wake wote aliokuwa nao Arsenal kwa kipindi hicho.

Hata hivyo alipotua Nou Camp tu, akaanza kukutana na kikwazo cha kupata namba kutokana na klabu hiyo kuwa na watu wao kwenye kiungo. Aliwakuta; Andres Iniesta, Xavi na Sergio Busquets ambao wanaonekana kuwa na ushirikiano mzuri.

Maisha yalianza kubadilika kwa kasi kwa Fabregas na kupoteza umaarufu wake tofauti na alivyokuwa kwenye Ligi Kuu England, ambapo alikuwa akitajwa kuwa moja ya wachezaji mahiri kabisa kwenye ligi hiyo.

Kwenye La Liga, Fabregas haonekani kuwa kama mchezaji makini ukiweka kando kwenye kikosi cha Barcelona peke yake. Fabregas anaonekana kuwa ni mchezaji wa kawaida sana. Ni kama hakuwahi kuwa nahodha wa klabu kubwa kabisa nchini England.
 http://static.guim.co.uk/sys-images/Guardian/Pix/pictures/2014/1/31/1391196340486/David-Moyes-Juan-Mata-008.jpg

Juan Mata


Wakati kocha, Jose Mourinho, alipomruhusu Juan Mata kuondoka  Stamford Bridge Januari mwaka huu kwenda Man United, jambo hilo liliwashangaza sana mashabiki kama ilivyokuwa kwa makocha wa timu nyingine pamoja na vyombo vya habari.

Si tu kwamba Mata alikuwa mchezaji bora wa Chelsea kwa misimu miwili mfululizo, bali ni kiungo mwenye ujuzi mkubwa sana wa kuuchezea mpira na kutengeneza nafasi uwanjani.

Kuhamia Man United kunatajwa kuwa pigo kwa Mata kwa sababu kwa kipaji chake, atashindwa kucheza Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao kutokana na nafasi ya timu yake mpya kwenye Ligi Kuu England kwa sasa.

Mata anashuhudia timu yake mpya ikikomea kwenye robo fainali kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya huku klabu yake ya zamani wa Chelsea ikiendelea kutesa kwenye michuano hiyo kwa kutinga nusu fainali.

Kuhitaji kucheza Kombe la Dunia nchini Brazil mwaka huu ndicho kitu kinachotajwa kumshawishi Mata kuhamia Man United kwa sababu Chelsea hakuwa hana namba na kuendelea kubaki kwenye klabu hiyo kungevuruga zaidi nafasi yake kwenye kikosi cha Hispania kitakachokwenda kwenye fainali za Kombe la Dunia nchini Brazil.
 http://www.howmanyarethere.net/wp-content/uploads/2012/12/fernando-torres-chelsea1.jpg


Fernando Torres


Staa huyo hahitaji maelezo mengi. Kila kitu kimejiweka bayana kwamba uhamisho wake wa pesa nyingi kwenye kikosi cha Chelsea umekuwa mbaya.

Fernando Torres alikuwa kwenye ubora mkubwa klabuni Liverpool na kwamba alikuwa na heshima mahali hapo, lakini kila kitu kimetibuka baada ya kuhamia Chelsea.

Torres amekuwa si tishio tena kwa mabeki wa timu pinzani tangu alipotua Stamford Bridge mwaka 2011. Straika huyo aliyewahi kuwa tishio kwenye kikosi cha Atletico Madrid, ameshindwa kurejesha makali yake ya zamani baada ya kutua Chelsea licha ya kwamba amekutana na makocha wengi wenye hadhi klabuni humo.
 http://metrouk2.files.wordpress.com/2012/08/article-1345214131027-1496761b000005dc-926530_636x418.jpg

Robin van Persie


Sawa, Robin van Persie, ametimiza dhamira yake ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu England baada ya kuhama kutoka Arsenal na kwenda Manchester United. Lakini, uhamisho huo si kitu ambacho kilitarajiwa kutokea mwanzoni.

Baada ya msimu mmoja kutesa, msimu uliofuata kocha Sir Alex Ferguson alistaafu ukocha Old Trafford na hapo Van Persie akaanza kupotea na kulalamikia mafunzo ya kocha mpya, David Moyes.

Kutokana na hilo, staa huyo msimu huu anahusishwa na mpango wa kurudi Arsenal na ripoti za kila siku zinazotawala mwenye vyombo vya habari ni kwamba Mdachi huyo hana furaha tena ya kubaki Old Trafford.
 http://soccerlens.com/files/2013/06/Neymar-Barca-flags.jpg

Neymar

Kwa sifa kubwa alizozipata akiwa bado na umri mdogo kabisa katika kikosi cha Santos, siku zote kilikuwa ni kitu kinachotarajiwa kwa staa wa Brazil, Neymar kwamba angehamia kwenye soka la Ulaya. Hilo lilitimia baada ya mchezaji huyo kuhamia Barcelona kwa pesa nyingi, huku klabu nyingine kama za Real Madrid na Chelsea nazo zikiwa zimesikitika kwa kuikosa saini yake.

Hata hivyo, Barcelona ambayo amekwenda kujiunga nayo si ile iliyokuwa chini ya kocha Pep Guardiola. Hii ya sasa imeshuka kiwango na Neymar anaonekana kuwa mzigo tu licha ya kwamba alipokuwa Santos alionekana kuwa mmoja wa mastaa wenye viwango vya maana duniani na kulinganishwa na wakali kama Lionel Messi na Cristiano Ronaldo.

Kiukweli kwenye soka la klabu, Neymar atakuwa anatamani kuzirudisha zama zake za klabuni Santos, ambapo alikuwa akitajwa kuwa staa wa kikosi hicho tofauti na ilivyo kwa sasa Barcelona, mahali ambapo Messi ana jina kubwa na timu hiyo inaundwa kwa kumtegemea Muargentina huyo.

Post a Comment

Previous Post Next Post