KAMPUNI YA BIA YA SERENGETI YAPATA MSHINDI WA TIKETI YA TATU YA KWENDA BRAZILI

  Meneja wa Bia ya Serengeti Rodney Rugambo(kulia) akizungumza na wana habari wakati wa droo ya Kumi na mbili  ya promosheni ya Winda Safari ya Brazili na Serengeti inayoendeshwa na Kampuni ya Bia ya Serengeti mara baada ya kuchezesha droo hiyo mapema leo katika ofisi za kampuni hiyo jijini Dar es Salaam na anayemshuhudia ni Afisa Mkaguzi kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha  Tanzania  Hummud Abdulhussen(kushoto).
 Meneja wa Bia ya Seregeti kutoka Kampuni ya Bia ya Serengeti Rodney Rugambo pamoja na Afisa Mkaguzi kutoka Bodi ya Michezo ya kubahatisha Tanzania Hummud Abdulhussen wakihakiki namba ya mshindi wa tatu wa tiketi ya kwenda Brazili wakati wa droo ya kumi na mbili ya Winda Safari ya Brazili na Serengeti. 
Meneja wa Bia ya Seregeti kutoka Kampuni ya Bia ya Serengeti Rodney Rugambo, akiongea na mshindi wa tatu wa tiketi ya Brazili kwa njia ya simu wakati wa droo ya mwisho ya promosheni ya Winda Safari ya Brazili na Serengeti jijini Dar es Salaam huku akishuhudiwa na afisa Mkaguzi kutoka Bodi ya Michezo ya kubahatisha Tanzania Hummud Abdulhussen.

Post a Comment

Previous Post Next Post