
Ferdinand, 35, anatarajiwa kuandika yote
yanayohusiana na maisha yake ya soka kwenye kitabu ambacho kitapewa jina
la ‘#2sides: Rio Ferdinand – My Autobiography.’
Kitabu chake kinatarajiwa kueleza kiundani
msimu mbovu kuliko yote ndani ya klabu hiyo kufuatia kuondoka kwa kocha
Alex Ferguson na timu kukabidhiwa kwa David Moyes ambaye alitimuliwa
wiki kadhaa zilizopita – huku wachezaji wakubwa kama Ferdinand wakitajwa
kuwa na mkono kwenye kutia mchanga kibarua cha Moyes.
Kitabu hicho kinatarajiwa kutoka October 2 na kinachapishwa na kampuni ya Blink Publishing.
إرسال تعليق