
“Watu wengi wanasema sisi ni watengenezaji filamu local ,lakini
zakwetu na za Kinaijeria hazina tofauti sana,kikubwa ambacho
kinasababisha kuamua sisi kutengezeza filamu local ni kipato, kwasababu
hata malipo yetu sisi na Wanaijeria ni vitu viwili tofauti, kwahiyo wao
wanauwezo wa kuagiza vyombo vya production vyenye quality nzuri
kwasababu wana uwezo wa kuilipa, akini pengine pesa kwangu mimi ya
kuwalipa na kufanyia filamu yote wao ni ya kuagiza equipment ya kufanya
movie moja, ndio maana sisi tunashindwa,” alisema Wastara.
Naye Riyama alisema:
“Wanasema umoja ni nguvu utengano ni udhaifu na katika tasnia yetu ya
filamu Tanzania umoja kwetu ni haba sana, ubinafsi, kuna umimi, sio ile
tufanye kitu kwaajili ya wote, kizazi cha leo,cha kesho na hata
kijacho, kwasababu mimi naamini kidole kimoja hakivunji chawa, siku zote
toka nimeingia kwenye tasnia ya filamu takriban miaka kumi na tano
inafika,lakini tumekuwa tukililia umoja ,umoja lakini umekuwa ukiishia
hewani.”
إرسال تعليق