Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kalambo, Dk Akilimali Mponzemenya alisema wanawake hao hao waliojifungulia kwa wakunga wa jadi kwa kipindi hicho cha miezi takribani mitano, ni asilimia 25 ya akina mama 2,685 waliojifungua katika vituo vya kutolea huduma ya afya wilayani humo.
Kwa upande wa huduma ya wagonjwa majumbani, Dk Mponzemenya alieleza kuwa idadi ya wagonjwa 560 ambao wanaishi na Virusi Vya Ukimwi, wanahudumiwa majumbani na kati yao wanaume ni 218 na wanawake 342.
Alizitaja baadhi ya changamoto zinazoikabili sekta ya Afya wilayani humo kuwa ni pamoja na baadhi ya akina mama kuendelea kujifugulia kwa wakunga wa jadi badala ya kwenda kwenye vituo vya kutolea huduma ya afya.
Changamoto zingine alizitaja kuwa ni uhaba wa watumishi wa afya wenye taaluma katika vituo vingi vinavyotoa huduma pamoja na upungufu wa vyombo vya usafiri yakiwemo magari na pikipiki .
Pia kitengo cha dawa wilayani humo hakina stoo ya kudumu kwa ajili ya kuhifadhia na hivyo dawa kutunzwa eneo lisilo rasmi.
Post a Comment