
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa 
Togo, Emmanuel Adebayor yuko safarini kwenda Kampala tayari kwa mechi ya
 wiki hii ya kuwania kufuzu fainali za mataifa ya Afrika, Afcon 2015 
dhidi ya Uganda The Cranes.
Siku chache zilizopita Adebayor 
hukuwepo kwenye kikosi cha Togo wakati wa mazoezi mjini Lome na hali hii
 ilizua wasiwasi kwamba angekosa mechi hiyo muhimu.
Hata hivyo, Supersport.com 
imethibitisha kuwa nyota huyo anayekipiga klabu ya Tottenham 
inayoshiriki ligi kuu soka nchini England amekuwepo Uganda asubuhi ya 
leo akitokea Nairobi.
Togo haina pointi yoyote kufuatia kupigwa 2-1 na Guinea mjini Casablanca na 3-2 kutoka kwa Ghana katika uwanja wao wa nyumbani.
Mechi dhidi ya Uganda ndio 
itatoa picha halisi ya nani ana nafasi kubwa ya kufuzu katika mashindano
 hayo yakayofanyika nchini Morocoo.
Post a Comment