Balozi wa Marekani afukuzwa katika kura Tunisia


Wananchi wa Tunisia leo wamemfukuza Balozi wa Marekani katika kituo kimoja cha kupigia kura kwenye uchaguzi wa bunge uliofanyika leo Jumapili nchini humo.
Wapiga kura huko Tunisia walipiga nara na kulaani uingiliaji wa Marekani na Qatar katika masuala ya ndani ya nchini mwao na hivyo kumfukuza Balozi wa Marekani aliyekuwa anatembelea kituo kimoja cha kupigia kura huko Tunis mji mkuu wa Tunisia.
Vyama, makundi na mirengo mbalimbali ya kiraia, vyama na shakhsia huru wa kisiasa wa
Tunisia viliwataka wananchi wa nchi hiyo kushiriki kwa dhati na kwa wingi katika uchaguzi wa leo wa bunge ili kufungua ukurasa mpya wa maisha ya wananchi na serikali nchini humo.
Weledi wa mambo wanaamini kuwa, kufanyika uchaguzi wa leo wa bunge huko Tunisia na kutangazwa matokeo yake kutahitimisha kipindi kilichojaa mivutano na hivyo nchi hiyo itakuwa imeingia katika kipindi kipya cha harakati za kisiasa na ujenzi mpya.

Post a Comment

أحدث أقدم