Kama unamfuata Wema Sepetu kwenye akaunti zake za mitandao ya
kijamii sina shaka uliona picha akiwa nje ya nchi hivi karibuni na timu
yake, hayo yote yalikuwa ni maandalizi ya msimu wa pili wa reality show
yake ya Tv ‘In My Shoes’.
Wema amesema msimu mpya utakuwa na maboresho mengi na surprises nyingi.
“Sasa hivi tumekuja kwa kasi flani hivi, wanasema mwanzo ni mgumu na season ya kwanza kiukweli ilikuwa ngumu lakini kuna mengi ambayo tumejifunza, kuna mabadiliko mengi, kwahiyo ni kama ime advance”. Wema ameiambia Power Jams ya EA Radio.
“Sasa hivi tumekuja kwa kasi flani hivi, wanasema mwanzo ni mgumu na season ya kwanza kiukweli ilikuwa ngumu lakini kuna mengi ambayo tumejifunza, kuna mabadiliko mengi, kwahiyo ni kama ime advance”. Wema ameiambia Power Jams ya EA Radio.
Kuhusu mpenzi wake Diamond kuonekana kwenye msimu mpya wa ‘In My Shoes’ wema amesema:
“Wote si tutamuona, yaani kwenye episode ya kwanza tu anaonekana,
so tutamuona, there will be a lot of Nasib kwasababu most of the times
ndio niko nae he is my baby kwahiyo tutaona vitu vingi vingi”.
Kipindi hicho ambacho huonesha maisha halisi ya Wema ambaye ni Miss
Tanzania wa mwaka 2006, hivi sasa kitakuwa kikiruka siku za Ijumaa
kuanzia saa tatu na nusu usiku kupitia EATV.
Post a Comment