TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) imeanza uchunguzi wa tuhuma za ufisadi wa Sh bilioni 40, uliotajwa kufanyika katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza.
Mkurugenzi
wa TAKUKURU, Dk Edward Hoseah alisema jijini Mwanza jana kuwa tayari
timu ya wachunguzi 148 wameshawasili jijini kuanza uchunguzi huo ambao
umekwishaanza, ingawa hakuweka bayana timu hiyo itakamilisha lini
uchunguzi huo.
“Tayari
Takukuru tumeshaleta timu ya mawakili wachunguzi 148 ambao wamepewa
jukumu la kuchunguza na kuendesha suala la ufisadi wa fedha katika jiji
la Mwanza”, alisema.
Hivi
karibuni Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa
nchini (LAAC) ilifanya ziara yake jijini Mwanza ambapo ilibaini
ubadhirifu wa Sh bilioni 40 na kutoa mapendekezo ya kufutwa kwa
jiji hilo kutokana na ubadhirifu huo.

إرسال تعليق