
Katibu wa Chama Cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa, Miraji Mtaturu
Na Mathias Canal, Mufindi
Katibu wa
Chama Cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa, Miraji
Mtaturu, amasema kuwa maendeleo ni mchakato na mipango sio kudanganya
wananchi kwa jambo lisilowezekana.
Aliyasema
hayo alipokuwa akiwahutubia wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa
kuimarisha chama Kijijini Kiyowela, Wilayani Mufindi.
"Maendeleo
ni mchakato mi sidhani kama kuna watu hapa ambao wamekamilisha kila
jambo katika familia zao, ila kila siku mnapanga na mnatekeleza jambo
moja baada ya jingine, sasa watakuja watu hapa watasema watawaletea kila
kitu kijijini kwenu, sasa kwa mtazamo wenu jambo hilo linawezekana
kweli? wananchi wakaitikia HAPANA"
Mtaturu
alitumia nafasi hiyo kuwapongeza wakazi hao kwa kumpitisha Endru Kapita,
kwenye kura za maoni za chama hicho ili kuiwakilisha Ccm kwenye
uchaguzi wa serikali za mitaa Disemba 14 mwaka huu.
Aliwataka
wananchi kujitokeza kujiandikisha kwenye daftari la mkazi ili waweze
kupiga kura kwani hiyo ni haki yao kikatiba kwa kila mtu mwenye sifa na
vigezo vya kupiga kura.(P.T)
"Ninawapongeza
kwa kufanya uchaguzi lakini leo tumempokea kijana mmoja kutoka Chadema
kwani Mwenda tezi na omo marejeo ngamani, hivyo kwa kuwa CCM ni nyumbani
tumpokee kwa heshima na taadhima kwakuwa sisi hatuna ubaguzi" Alisema
Mtaturu
Aidha
aliwataka wananchi hao kuwaepuka baadhi ya watu ambao wanapita mitaani
kuwapotosha ili wasiikubali katiba mpya, ambayo imekidhi matakwa ya
wananchi wote kuanzia wafugaji, wakulima na nyanja zingine nyingi.
"Kila
mwenye macho haambiwi tazama hivyo ninawaomba kuisoma katiba na kuielewa
ndipo muipigie kura ya ndio kwa kuwa imekidhi matakwa ya watanzania,
Kumbukeni mnaweza kujaribu nguo,chakula,malazi na mavazi lakini uongozi
haujaribiwi ni kama kujaribu kuonja sumu" Alisisitiza Mtaturu
Akijibu
swali la Andrea Simwiche aliyetaka kujua juu vijana waliomaliza kidato
cha nne kusimamia uchaguzi wa serikali za mitaa, Mtaturu alisema kila
mtanzania ana haki ya kufanya kazi kama ana uwezo wa kufanya kazi endapo
tu kama atakuwa hajavunja sheria za kazi.
"Jambo
hili nimelichukua nitalifanyia kazi ili kila mmoja apate ajira kwa
mujibu wa sheria, lakini nimesikia watu wakisema sema kuhusu wagombea,
naomba niwatoe wasiwasi kwamba mgombea atakaye shinda kura za maoni
ndiye atakayepigiwa kura tarehe 14 Disemba, hivyo mimi sitambadilisha
mjumbe yeyote yule kwa matakwa yangu ama ya mtu mwingine"
Hata
hivyo Mtaturu aliwasihi viongozi wanaomaliza muda wao serikalini kupitia
Chama Cha Mapinduzi, kushirikiana na kila mgombea sambamba na wananchi
ili waweze kupata kiongozi anayependwa na kukubalika na jamii yake kwa
ajili ya maendeleo ya kijiji na Taifa kwa ujumla.
إرسال تعليق