Wahitimu Veta waililia serikali

 
SERIKALI imeobwa kulegeza masharti ya upatikanaji wa leseni za kufungua kampuni ili kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa ajira kwa vijana wanaohitimu mafunzo ya ufundi stadi (VETA).
Ombi hilo limetolewa mjini hapa juzi na wahitimu wa chuo hicho wakati wa mahafali ya 38 chuo hicho ambao walisema hivi sasa ni vigumu kupata ajira serikalini hivyo kutumia ujuzi wao kufungua kampuni zitakazowapa ajira na kuwaletea maendeleo.
“Tunajivunia kumaliza kozi zetu ila changamoto kubwa iko katika kupata ajira iwe serikalini ama taasisi binafsi  kutokana na kuwa na wasomi wengi ambao hawana kazi,” alisema Salim Ramadhani.
Kwa upande wake mkuu wa chuo cha ufundi stad veta Injinia Alfhonce Rubasha alisema wanakabiliwa na changamoto ya upungufu wa madarasa kutokana na ongezeko la wanafunzi.
Mkuu huyo wa Veta jijini hapa aliwaeleza wazazi na walezi kwamba vyuo vya ufundi vinaweza kuwabadilisha watoto wao waliokosa nafasi ya kuendelea na masomo katika mfumo rasmi hivyo kuwatambua kwa ujuzi wao.
Naye Ofisa Elimu Sekondari wa Jiji la Tanga, Bashiru Shelimo alisema wapo wanafunzi wengi wanaomaliza sekondari wanakata tamaa na kusahau kwamba vyuo vya ufundi vinaweza kuwatoa kimaisha kama vilivyo vyuo vyengine.
- Tanzania Daima

Post a Comment

أحدث أقدم