Watu sita wamefariki dunia baada ya kupigwa na radi na wawili kujeruhiwa wilayani Songea.

Watu wasita wamefariki dunia na wengine wawili kujeruhiwa wilayani Songea mkoani ruvuma  baada ya  kupigwa na radi Kufuati mvua kubwa iliyonyesha usiku huo.
Kamanda wa polisi wa mkoa wa ruvuma ACP Mihayo Msikhela amesema kuwa Maafa hayo yalitokea majira ya saa  mbili usiku wakati watu hao
Wakila chakula cha usiku kwenye  mgahawa wa chuo cha kilimo na mifugo Cha liti madaba songea  na kwamba mvua kubwa ilinyesha  majira ya saa
Moja na nusu hadi saa mbili na baadaye ikapiga radi na kuua watu sita Na kujeruhi watu wawili.
Amewataja walipopoteza maisha kwa kupigwa na radi kuwa ni Chesco Luoga mwanafunzi wa chuo cha liti madaba na mkazi wa Ludewa,Lucas
Mabula mwanafunzi wa chuo hicho na mkazi wa magu mkoani mwanza,Eva Chapile,muhudumu wa mgahawa wa chuo hicho,Osiana Antoni mhudumu wa
Mgahawa wa chuo hicho,Justine Ngonyani mkulima na mkazi wa madaba Songea na Edwini Fungo mkulima na mkazi wa madaba songea.
Amewataja majeruhi kuwa ni Beatrice Mhagama mwanafunzi wa chuo cha Kilimo na mifugo liti madaba na mkazi wa peramiho songea na Leokadia
Fusi muhudumu wa mgahawa wa chuo hicho na kwamba miili ya marehemu na majeruhi wako katika kituo cha afya madaba.
Kutokana na  tukio hilo mkuu wa mkoa wa Ruvuma Bw.Said Mwambungu  na Mkuu wa wilaya ya songea Bw.Joseph Mkiriki wameenda eneo la tukio
Madaba songea na kueleza kusikitishwa na tukio hilo na kusema huo ni msiba  mzito kwa mkoa wa Ruvuma
- ITV

Post a Comment

أحدث أقدم